Ofisa Uhusiano Kampuni ya Bia
Tanzania (TBL), Dorris Malulu, akikata utepe kuashiria uzinduzi wa
kisima kilichojengwa kwa msaada wa kampuni hiyo katika Zahanati ya NBC
Tabata, Dar es Salaam. Kisima hicho kilizinduliwa na Mwenyekiti wa
Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii Ilala, Angelina Malembeka. Kushoto
ni Mganga Mkuu wa Ilala, Willy Sangu na anayefuatia ni Mwakilishi wa
Mkurugenzi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Dk Assenga Severine na
kulia ni Mganga Mfawidhi Zahanati ya Tabata NBC, Catherine Akili.
Wauguzi wa Zahanati ya Tabata
NBC, Dar es Salaam, wakishangilia baada ya Ofisa Uhusiano Kampuni ya
Bia Tanzania (TBL), Dorris Malulu kukabidhi msaada wa kisima kwa
zahanati hiyo.
Malulu akizungumza wakati wa hafla hiyo ya makabidhiano.
Baadhi ya wakazi wa Tabata waliofika kwa kupata huduma za tiba katika Zahanati hiyo wakishiriki katika hafla hiyo.
Mwakilishi wa Mkurugenzi
Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Dk Assenga Severine, akifungua pazia
kuashiria kuzindua rasmi kisima katika Zahanati ya Tabata Nbc Dar es
Salaam.
Ofisa Uhusiano kampuni
hiyo,Dorris Malulu, akimkabidhi ufunguo wa kisima hicho Mwakilishi wa
Mkurugenzi Halmashauri ya Manispa ya Ilala, Dk. Assenga Severine,
kuashiria Uzinduzi wa Kisima ambacho kimejengwa kwa msaada wa TBL.
Mkurugenzi Halmashauri ya
Manispa ya Ilala, DK Assenga Severine na Ofisa Uhusiano kampuni ya Bia
Tanzania Breweries (Tbl),Dorris Malulu wakionja maji ya kisima hicho
baada ya Kuzindua kisima hicho.
Mkurugenzi Halmashauri ya
Manispa ya Ilala, Daktari Assenga Severine akimsaidia kumtwisha ndoo ya
maji Ofisa Muuguzi wa zahanati yiho Flora Amos.
Ofisa Uhusiano kampuni ya Bia
Tanzania Breweries (Tbl),Dorris Malulu, akimsaidia kumtwisha ndoo ya
maji mmoja wa Wauguzi wa Zahanati hiyo
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269