Mamia
ya wapenzi na washabiki wa klabu kongwe ya mpira wa miguu hapa nchini
Simba leo mchana wamejikusanya kwa wingi katika makao makuu ya klabu yao
hiyo,kupinga Michael Wambura kuondolewa kwenye orodha ya wagombea
kwenye uchaguzi unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.Wanachama hao ambao
walizunguka jengo hilo na kutaka wapewe sababu za msingi kwanini
Wambura ameondolewa huku wakitaka kufanya vurugu lakini vyombo vya
usalama waliwahi kufika eneo la tukio na kuweza kuwatuliza wanachama
Hao.
Polisi
wakiwa wamefika eneo la klabu ya simba ili kuimarisha ulinzi na
kuwataka wanachama wa simba kutulia ili wapate majibu kwa kamati ya
uchaguzi.
Wanachama
wa simba wakiwa wamelizunguka Jengo la klabu yao mchana huu kupinga
kuondolewa kwa wambura kwenye uchaguzi wa klabu hiyo.Picha na Sek David
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269