Breaking News

Your Ad Spot

May 29, 2014

WANACHAMA WA SIMBA WAANDAMANA NA KUFUNGA NJIA YA MSIMBAZI WAKITAKA WAMBURA ARUDISHWE KWENYE ORODHA YA WAGOMBEA

Mamia ya wapenzi na washabiki wa klabu kongwe ya mpira wa miguu hapa nchini Simba leo mchana wamejikusanya kwa wingi katika makao makuu ya klabu yao hiyo,kupinga Michael Wambura kuondolewa kwenye orodha ya wagombea kwenye uchaguzi unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.Wanachama hao ambao walizunguka jengo hilo na kutaka wapewe sababu za msingi kwanini Wambura ameondolewa huku wakitaka kufanya vurugu lakini vyombo vya usalama waliwahi kufika eneo la tukio na kuweza kuwatuliza wanachama Hao.
 Polisi wakiwa wamefika eneo la klabu ya simba ili kuimarisha ulinzi na kuwataka wanachama wa simba kutulia ili wapate majibu kwa kamati ya uchaguzi.
 Wanachama wa simba wakiwa wamelizunguka Jengo la klabu yao mchana huu kupinga kuondolewa kwa wambura kwenye uchaguzi wa klabu hiyo.Picha na Sek David

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages