Breaking News

Your Ad Spot

Jun 27, 2014

FARIDA FOUNDATION YATOA MISAADA HOSPITALI YA PALESTINA SINZA NA KWA WALEMAVU ENEO LA UBUNGO DARAJANI

 Mkurugenzi wa Farida Foundation akikabidhi moja ya msaada kwa kaimu Mganga mkuu wa Hospitali ya Palestina Dk Hugoline Mselle,Huku wafanyakazi wengine wa Hospitali hiyo wakishuhudia.
 Bi Farida Abdul Akikabidhi bandeji kwa ajili ya kufungia wagonjwa kwa Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Palestina Dk Hugoline Mselle
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Palestina Dk Hugoline Mselle akipoke Ndoo zitakazotumika kwa ajili ya kuhifadhia uchafu katika Hospitali hiyo,ambazo zilitolewa kama Msaada na Farida Foundation
 Bi Farida Abdul akimuonyesha kaimu Mganga mkuu wa Hospitali ya Palestina Dk Hugoline Mselle Vifaa ambavyo vimeletwa kama msaada kwenye Hospitali hiyo.Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na Viti vya magurudumu vitatu ambavyo vitasaidia kubebea wagonjwa,Bandeji za kufungia vidonda,Ndoo za kuwekea taka,na vinginevyo.
 Hivi ni viti Vitatu vya kubebea wagonjwa ambavyo vilitolewa kama msaada kwenye Hospitali ya Palestina(sinza) na Farida Foundation.
 Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Palestina Akimshukuru Bi Farida Abdul kwa kutoa msaada katika hospitali hiyo na akampongeza kwa moyo wake na kumsisitiza aendelee Kusaidia kila mara anapopata nafasi ili huduma zao ziwe bora zaidi kila siku.
 Mkurugenzi wa Farida Foundation Bi Farida Abdul akiongea na vyombo vya habari na kuelezea ni kwanini ameamua kutoa misaada hiyo katika hospitali ya Palestina,Amesema kwamba Serikali peke yake haiwezi kufika kwa kila mgonjwa na hospitali kwa wakati,kwa hiyo inatakiwa kujitoa kwa mashirika kusaidiana na Serikali ili Hospitalietu Ziweze kuwa na Huduma bora.
Kaimu mganga Mkuu wa Hospitali ya Palestina Dk Hugoline Mselle ameishukuru Taasisi ya Farida Foundation kwa misaada waliyotoa kwani itawasaidia sana kuboresha Huduma zao.

BAADA YA KUTOKA HOSPITALI YA PALESTINA SINZA FARIDA FOUNDATION WALIELEKEA UBUNGO DARAJANI KWA AJILI YA KUTOA MSAADA KWA MLEMAVU WA MIGUU,AMBAPO WALIMPATIA BAISKELI NA MTAJI WA VITU VYA BIASHARA
 Mkurugenzi wa Farida Foundation Bi Faridah Abdul akiongea na mlemavu wa miguu ndugu Marcerine Mayemba eneo la ubungo darajani kabla ya kumkabidhi msaada wa mtaji wa biashara pamoja na baiskeli atakayokuwa anaitumia.
 Bi Farida Abdul Akiwa na baiskeli ambayo aliikabidhi kwa mlemavu wa miguu bwana Marceline Mayemba,kwa ajili ya kumsaidia katika matumizi yake ya kila siku
 Mlemavu wa Miguu Bwana Marceline Mayemba Akipanda kwenye Baiskeli yake aliyokabidhhiwa na Farida Foundation
 Mlemavu wa Miguu Bwana Marceline Mayemba Akiendesha Baiskeli yake mara tu baada ya kukabidhiwa na Farida Foundation
 Bi Farida Abdul Akimkabidhi Mlemavu wa miguu bwana Marceline Mayemba Katoni ya Bidhaa ambazo ataanza nazo kama mtaji wa bishara,pia alikabidhiwa katoni tatu za maji,Katoni tatu za Juice na Katoni zingine Vifaa kama pipi,bigijii ili viwe kama kianzio kwa biashara yake.
Bi Farida Abdul Mkurugenzi wa Farida Foundation akikabidhi Mlemavu mwingine Chakula Pamoja na vinywaji.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages