Breaking News

Your Ad Spot

Jul 15, 2014

WAUMINI WAFUNGA OFISI ZA ASKOFU KUSHINIKIZA AJIUZULU!!!

Mmoja wa waumini wa kanisa  la Moravian Tanzania jimbo la Kusini Maghalibi akiweka sawasawa minyororo katika lango la kuingilia jimboni hapo eneo la jakaranda jijini mbeya ikiwa na lengo  la kushinikiza Askofu Mkuu wa Kanisa hilo Alinikisa Cheyo kujiudhuru .Picha na Keneth Ngelesi
Mmoja wa wachungaji wa kanisa hilo akiweka bayana lengo la wawo kuweka kambi jimboni hapo.
Jeshi la Polisi nalo halikuwa mbali kuimalisha ulinzi na usalama katika eneo hilo la tukio




Baadhi ya waumini na wachungaji wa kanisa hilo wakiendelea na mapambio nje ya kanisa hilo kama walivyo kutwa na mpiga picha wetu.






Makamu Mwenyekiti wa kanisa hilo Ndugu Zakalia Schone akizungumzia sakata hilo.

wafanyakazi wakiwa hawaamini kinachotokea jimboni hapo 

Baadhi ya wafanyakazi wa jimbo hilo wakiwa nje ya ofisi zao kwa zaidi ya masaa Manne  mara baada ya kuzuiliwa kuingia ndani ya ofisi zao na waumini hao ambao wameweka kambi  jimboni hapokwa lengo la kushinikiza Askofu wa Kanisa hilo kujiuzulu.

jeshi la polisi wakiwa katika doria nje ya kanisa hilo

Baadhi ya wachungaji wa shirika mbalimbali mkoani mbeya katika kanisa la Moravin wakiwa nje ya kanisa hio kusubiri hatma ya mgogoro wao na Askofu Mkuu wa jimbo hilo kujiudhuru kwa madai mbalimbali.
Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mbeya Ndugu Richard Mchomvu akizungumza na waumini hao kwa lengo kusitisha maamuzi yao ya kuendelea kuzifunga ofisi hizo za jimbo.

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalaama Dakta Nouman Sigala akiwasihi waumini na wachungaji waliweka kambi nje ya kanisa hilo na kufunga milango ya ofisi zote za jimbo kulegeza msimamo wao na kuluhusu huduma kuendelea mpaka pale uongozi wa kanisa hilo utakapo kutana na kujadili hatma ya mgogoro huo ambao ni kesho(julai 15) mwaka huu.
Wachungaji na waumini wa kanisa hilo wakifanya maombi ya pamoja mara baada ya kumaliza kumsikiliza Mkuu wa Wilaya Dakta Nouman Sigala  nje ya uzio wa kuingilia Kanisani hapo.
Na EmanuelMadafa,Mbeya
Katika hali isiyokuwa ya kawaida waumini wa Kanisa  la Moravian Tanzania  Jimbo la Kusini Magharibii, leo wamezifunga ofisi za Jimbo hilo zilizopo eneo la jacaranda jijini Mbeya , wakishinikiza  kujiudhulu kwa Askofu  wa Jimbo hilo Alinikisa Cheyo kujiudhuru wadhifa wake.

Madai mengine ya waumini na wachungaji hao ni  pamoja kushinikiza kuitishwa kwa halmashauri ili waitishe   Sinodi ambayo ndiyo yenye maamuzi ya mwisho kuhusiana na mgogoro huo.

Hatua hiyo ya kuzifunga ofisi hizo, imekuja ni baada ya kuwepo kwa mgogoro  uliodumu kwa mwaka mmoja na nusu ukihusisha  ofisi ya halmashauri Kuu ya Jimbo la Kusini Magharibi dhidi ya Mchungaji na Mwenyekiti wa Jimbo hilo Nosigwe Buya na  Askofu Alinikisa Cheyo.

Waumini wa Kanisa hilo pamoja na wachungaji, wamekuwa wakimtuhumu Askofu wa jimbo hilo ya kwamba amekuwa akikiuka Katiba ya Kanisa kwa kuingilia baadhi ya shughuli ambazo hazimuhusu.

Moja ya mambo yanayotajwa kuingiliwa na Askofu huyo yakiwa ni kinyume cha taratibu na sheria zilizomo kwenye Katiba yao ni kufanya maamuzi ya kumsimamisha kazi aliyekuwa Mwenyekiti wa jimbo hilo Mchungaji Buya kinyume cha taratibu.

Wakizungumza katika eneo la tukio    baadhi ya waumini na wachungaji ambao walikuwa kwenye eneo la tukio, wamesema Askofu  Cheyo amekuwa akisahau wajibu na majukumu yake ya kiroho na ushauri na kuingilia masuala ya  kiutendaji zaidi.

Wamesema,  hali hiyo inatokana na dhamira mbaya aliyokuwa nayo  askofu huyo  ya kutaka kufanya jaribio la kumuondoa Mwenyekiti Mchungaji Nosigwe Buya huku akijua kabisa anafanya makosa kikatiba kwa kufanya mapinduzi.

Akisimulia chanzo cha sakata hilo kutokea Mchungaji Chile amesema,  mgogoro huo ulianza 30/4/2014 ambapo halmashauri kuu ilikutana na kujadili agenda juu ya utendaji mbovu wa kamati tendaji  na katika kikao hicho walimtaka Mwenyekiti kutoa tahalifa ya  shilingi milioni 200 ambazo zilikuwa za ujenzi wa Sekondari ya Mbozi.

Pia, Makamu wa kanisa hilo Zakaria Sichone kutakiwa  kuwasilisha taarifa ya maandishi ya jinsi alivyotimiza wajibu wake kikatiba ya kusimamia ujenzi wa majengo hayo ya shule lakini taarifa hiyo ilikataliwa kutokana na kuwepo kwa kasoro nyingi.

Amesema, wakiwa ndani ya kikao hicho, Askofu Cheyo aliamuru Mwenyekiti Buya  na Makamu wake watoke nje ya kikao jambo ambao ni kinyume cha Katiba kwani yeye nafasi yake ni kushauri na si kufanya maamuzi kama mjumbe.

Amesema, Askofu huyo tena akiwa anafahamu Katiba ya Kanisa inasema nini, alishindwa kutoa ushauri kwa wajumbe walioshiriki kikao cha kuwajadili Mwenyekiti Buya na makamu wake ambacho kilitoa maamuzi ya kuwatoa nje kisha kufanya uchaguzi mpya na kumchagua Mwenyekiti   Hakimu Mwandanuka kukalia kiti hicho.

Aidha, waumini hao ambao walizifunga ofisi hizo kwa zaidi ya masaa matano waliweza kuzifungua baada ya kuwasili kwa  Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Nomarn Sigalla ambaye aliwaomba kutulia kwani serikali inalifahamu tatizo hilo na kwamba imepanga kukutana na uongozi wa pande zote mbili(kesho) leo..

Mgogoro huo umeleta madhara makubwa katika kanisa ambao mpaka sasa waumini na watendaji wa halmashauri ya jimbo hilo wamegawanyika na kuleta uhasama dhidi ya mchungaji na mchungaji, ushirika na ushirika hivyo wachungaji kuwa na waumini wao hali inayoleta uvunjifu wa amani ndani ya kanisa na nchi kwa ujumla

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages