Breaking News

Your Ad Spot

Aug 23, 2014

WASANII WATAKAOTUMBUIZA TAMASHA LA FIESTA 2014 JIONI YA LEO JIJINI TANGA WAMJULIA HALI MZEE NJENJE NYUMBANI KWAKE SAHARE

 Mwanamuziki Mkongwe hapa nchini,almaarufu kama Mzee Njenje akizungumza machache mbele ya wasanii mbalimbali wa bongofleva waliofika nyumbani kwake Sahare,nje kidogo ya jiji la Tanga,kumjulia hali kutokana na maradhi yake yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda sasa.

Mzee Njenje amewaasa wasanii hao ambao amekiri wazi kuwa wanafanya vizuri katika anga ya muziki wao,kupata muda mwingi wa kupumzika ikiwemo na suala la kutoendekeza masualaua ya anasa kama vile ulevi,ngono na mengineyo ambayo huchangia kuporomoka kwa wasanii wengi,amesema kuwa Muziki wa sasa una ushindani mkubwa hivyo kila msanii anapaswa kujituma kwa namna anayoona inafaa ili kutimiza malengo yake sambamba na kuitangaza nchi kwa ujumla.
 Wasanii wa Muziki wa Kizazi kipya,Rachael na Linah wakiwa wamepozi katika picha ya ukumbusho na Mzee Njenje.
 Msanii wa muziki wa Kizazi Kipya,Alli Kiba akizungumza jambo na Mzee Njenje. 
Mzee Njenje akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya watakaotumbuiza jioni ya leo kwenye tamasha la Fiesta 2014 linalofanyika kwenye uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga,Wasanii hao walikwenda kumsabahi mkongwe huyu wa Muziki hapa nchini,Nyumbani kwake Sahare,nje kidogo ya jiji la Tanga ambako ndiko anaendelea kupata matibabu yake ya maradhi yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda sasa,Mzee Njenje amesema kuwa kwa sasa anamshukuru Mungu anaendelea vizuri na afya yake inazidi kuimarika kadiri ya siku zinavyozi kwenda.  
 Baadhi ya Wasanii mbalimbali ambao Watatumbuiza kwenye tamasha la Fiesta jioni ya leo ndani ya uwanja wa Mkwakwani ,wakiwasili nyumbani kwa Mzee Njenje,Sahare,nje kidogo ya jiji la Tanga kumjulia hali.Picha zote na Michuzi Jr-FIESTA TANGA

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages