Breaking News

Your Ad Spot

Sep 29, 2014

KINANA ATINGA BUMBULI, ANG'AKA KIWANDA CHA CHAI KUFA MPONDE, ATAKA VIONGOZI WALIOHUSIKA WAWAJIBISHWE.


Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi katika kata ya Mponde, akiwa katika ziara ya kukagua na kusimamia utekelezaji wa ilani ya CCM, kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia ya kuzitatua, katika jimbo la Bumbuli, wilayani Lushoto mkoani Tanga, leo, Septemba 29, 2014.
      Akizungumza na mamia ya wananchi waliofurika kwenye viwanja vya Kijiji cha Mponde, Kinana ameitaka serikali kuwachukulia hatua za kisheria viongozi wote waliohusika kwa namna moja au nyingine kusababisha kiwanda cha Chai cha Mponde, kufa baada ya kubinafsishwa kwa njia zinazoashiria kutofuata utaratibu unaotakiwa.
     Pia Kinana ameahidi kulifikisha suala hilo katika vikao vikubwa ikiwemo cha Kamati Kuu ya CCM, ili kuhakikisha unapatikana ufumbuzi wa kero hiyo ikiwemo kuwachukulia hatua viongozi waliohusika.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimia wananchi baada ya kuwasili katika kijiji cha Mbuzii kushiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM kata ya Mbuzii, katika jimbo la Bumbuli, wilayani Lushoto mkoa wa Tanga, leo Septemba 29, 2014. Kushoto ni Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akijadili kwa makini jambo na Mbunge wa Bumbuli, Waziri Januari Makamba, wakati wa kushiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM Kata ya Mbuzii, jimboni humo, leo, Septemba 29, 2014.
 Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba akizungumza wakati wa makaribisho ya katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akushiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM, Kata ya Mbuzii jimboni humo mkoani Tanga, leo Septemba 29, 2014. pamoja naye ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
 Katibu wa NEC, Itikadi na uenezi, Nape Nnauye akizungumza wakati wa makaribisho ya Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana (Wapili kushoto), kushiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM Kata ya Mbuzii, katika jimbo la Bumbumuli, Lushoto mkoani Tanga leo Septemba 29, 2014. Watatu kushoto  ni Mbunge wa jimbo hilo, Januari Makamba.
 Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba (kulia) akimuonyesha Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana eneo la Ofisi ya CCM Kata ya Mbuzii, linalojengwa pamoja na ukarabati wa ofisi ya zamani ya Chama ambayo ilikuwa imechakaa kutokana na kuwa ya muda wa miaka mingi tangu enzi za Tanzania kupata Uhuru
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki Ujenzi wa Ofisi ya CCM Kata ya Mbuzii, leo Septemba 29, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCm na kukagua uhai wa Chama katika jimbo la Bumbuli wilayani Lushoto mkoa wa Tanga. Kulia ni Mbunge wa jimbo hilo, Januari Makamba akifanya 'kibarua' cha kumpa tofali Kinana..
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikagua jengo la zamani la Ofisi ya CCM Kata ya Mbuzii ambalo linafanyiwa upanuzi na ukarabati, alipofika kushiriki ujenzi wa Ofisi hiyo, leo katika jimbo la Bumbuli mkoani Tanga. Nyuma yake ni Mbunge wa jimbo hilo, Januari Makamba
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrah,man Kinana akisalimiana na Mzee aliyesema kwamba amewahi kuwa dereva wa wakoloni, alipokutana na Kinana aliyewasili kushiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM Kata ya Mbuzii, jimbo la Lushoto mkoa wa Tanga.
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimkabidhi fungua na hati za pikipiki, kiongozi wa madereva wa Bodaboda katika kijiji cha Dule B, Kata ya Mbuzii wilyani Lushoto mkoa wa Tanga. Pikipiki hiyo imetolewa na Mbunge wa Bumbuli, January Makamba.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwatazama Katibu wa NEC, Itikasi na Uenezi, Nape Nnauye na Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba wakiendesha pikipiki za waendesha bodaboda wa Kijiji cha Dule B, Kata ya Mbuzii, katika jimbo hilo wilayani Lushoto mkoa wa Tanga.

Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Majid Mganga akiendesha boda boda wakati msafara ukienda kwenye uzinduzi wa shina la wajasiriamali la Maisha Plus kata ya Dule.
 Gari la Maofisa wa CCM na Waandishi wa habai walioko kwenye msafara wa katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana likiwa limevunjika kioo baada ya gari hilo kukwaruzana na lingine, wakati msafara ulipowasili katika Kijiji cha Dule B, kuzindua shina la wakereketwa wa CCM ambao ni wajasriamali wa mradi wa kufyatua matofali wa Kikundi cha Maisha Plus. Hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo.
 Mbunge wa Jimbo la Bumbuli ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba akiwasalimu wajasiriamali wa Maisha Plus wakati wa ziara ya Katibu mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana .
 Wakazi wa kata ya Dule B wakisikiliza kwa makini hotuba za viongozi wao kabla ya kuzinduliwa kwa shina la wajasiriamali la Maisha Plus.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwasalimu wajasiriamali wa Maisha Plus ambapo alizindua shina la CCM wajasiriamali wa Maisha Plus katika kata ya Dule B
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kupasua mawe kwenye kambi ya Maisha Plus ,jimbo la Bumbuli wilaya ya Lushoto mkoani Tanga.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishiriki kufyatua matofali .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijiandaa kuukata muwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Mheshimiwa January Makamba
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akila muwa, Maisha Plus
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimuelekeza  Mbunge wa Jimbo la Bumbuli January Makamba namna ya kupiga randa  kwenye Kituo hicho cha Maisha Plus.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akipandisha bendera ya CCM  kuzindua shina la wakereketwa Wajasriamali wa CCM Kikundi cha Maisha Plus, eneo la Dule B ,jimbo la Bumbuli wilaya ya Lushoto.
 Maisha Plus Bumbuli.
 Abdulkarim Jambia aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema kata ya Vuga akionyesha juu kadi yake ya CCM baada ya kurejea rasmi CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Mponde.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akijionea namna mashamba ya chai yalivyogeuka vichaka . Katibu Mkuu ameongozana na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Mheshimiwa January Makamba.
 Mamia ya wananchi wakiwa wamefurika kwenye mkutano wa hadhara aliohutubia Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, katika Kata ya Mponde, jimbo la Bumbuli wilayani Lushoto mkoani Tanga, leo Septemba 29, 2014.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia kwenye mkutano huo wa Kinana
 Baadhi ya watu wakiwa wamekaa ,kilimani kuhakikisha wanamuona Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akipohutubia Mkutano wa hadhara katika Kata ya Mponde kwenye jimbo la Bumbuli mkoani Tanga leo.
 Mbunge wa Bumbuli Januari Makamba akieleza kero kuhusu zao la chai na kufa kwa kiwanda cha Chai cha Mponde, alipokaribishwa na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akuzungumza na wapigakura wake.
Mwananchi wa Mponde akieleza kwa hisia, jinsi wananchi wa Bumbuli wanavyosumbuliwa na kero ya kufa kiwanda cha Chai kilichopo Kata ya Mponde kwa miaka mingi sasa. Asilimia kubwa ya wakazi wa Bumbuli ni wakulima wa Chai. Picha zote na Bashir Nkoromo-theNkoromo Blog

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages