Breaking News

Your Ad Spot

Dec 22, 2014

JK AMNG'OA UWAZIRI PROFESA TIBAIJUKA SAKATA LA TEGETA ESCROW


 Mh.Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na taifa kupitia Wazee wa Dar es Salaam leo katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik na kulia ni katibu wa Baraza la wazee wa Dar es Salaam Abdul Mtulia.Rais alizungumzia sauala ya vurugu katika uchaguzi wa Srikali za Mitaa na kuagiza vyombo vya kuwachukulia hatua za kisheria. Vilevile alifafanua kuhusu sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow na kuchukua uamuzi wa kumng'oa aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na kumuweka kiporo Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

 Baadhi ya mawaziri wakisikiliza kwa makini hotuba ya Rais Jakaya Kikwete, ambapo alifafanua kuhusu sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow na kutangaza kumg'oa uwaziri aliyekuwa  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na kumuweka kiporo Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

 Baadhi ya wazee na wananchi wakimsikiliza kwa makini Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipokuwa akilihutubia taifa kupitia wazee wa Dar es Salaam katika ukumbi wa  Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam leo

 Wazee wa Wilaya ya Temeke wakiwa katika mkutano huo

 Sehemu ya umati wa wananchi wakiwa kwenye mkutano huo



Baadhi ya viongozi wa dini wakiwa katika mkutano huo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages