Breaking News

Your Ad Spot

Dec 4, 2014

WAHITIMU 130 CHUO KIKUU CHA ARDHI (ARU) WAPATA TUZO KWA KUFANYA VIZURI KATIKA MASOMO


 Onesmo Charles ambaye ni mmoja wa wanafunzi 130 waliofanya vizuri katika masomo katika Chuo Kikuu cha Ardhi (ARU), akijaribu kifaa cha kisasa cha kupimia ardhi, viwanja na ramani za nyumba alichozawadiwa Kampuni ya Hightech Systems (T) Limited katika hafla ya kuwakabidhi zawadi na tuzo wanafunzi hao bora  iliyofanyika katika chuo hicho leo ikiwa ni sehemu ya mahafali ya nane ya chuo hicho yatakayofikia kilele kesho kutwa Ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam.

 Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi Dar es Salaam (ARU), Idrissa Mshoro (kulia) akimkabidhi mwanafunzi Onesmo Charles kifaa cha kisasa cha kupimia ardhi, viwanja na ramani za nyumba chenye thamani ya sh. mil. 35  baada ya kuwa mmoja wa wanafunzi 130 waliofanya vizuri katika masomo. Hafla ya kuwakabidhi zawadi wanafunzi hao bora  iliyofanyika katika chuo hicho leo, ni sehemu ya mahafali ya nane ya chuo hicho yatakayofikia kilele kesho kutwa kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Godfrey Ntaki wa Kampuni ya Hightech Systems (T) Limited.  iliyotoa zawadi hiyo. (PICHA ZOTE NA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG)

 Onesmo akipongezwa na wanafunzi wenzake

 Onesmo akiwa katika picha ya pamoja na wenzake

 Cheti alichotunukiwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

 Ipyana Mwangoka akikabidhiwa zawadi ya cheti

 Jonathan Kansheba akitunukiwa cheti

 Joyce Kasenga akipatiwa tuzo ya cheti

 Mariam Maringe akipatiwa tuzo

 Rashid Ngenyi akipatiwa tuzo ya cheti

 Rebecca Milano alipatiwa tuzo tano

 Tadeus Rudaichi akipokea tuzo

 Asha Muhali alituzwa tuzo tano

Anthony Mwashilingi akizawadiwa

 Bibian Abel akizawadiwa

 Faraja Ally akizawadiwa cheti

 Ikupa Mwakisole akipokea tuzo ya cheti





 Sehemu ya wanafunzi waliotunukiwa tuzo

 Meza kuu

 Wanafunzi wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa chuo hicho pamoja na wafadhili




No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages