Kumekuwa na matukio mengi yanayotokea
ndani ya Mabunge mbalimbali duniani halafu yanachukua headlines kubwa
mtaani na mitandaoni, tumeona ya TZ, Kenya, Afrika Kusini ile juzi
wakati Rais Zuma akiwa anahutubia, hii nakupa na wewe uipate kutoka
ndani ya Mjengo wa Bunge Canada.
Mbunge Pat Martin naye katoa kali ya mwaka, ile story yake aliyoitoa yani hakuna Mbunge ambaye hakucheka.
Kulikuwa na
ishu ya kupiga kura ikiendelea ndani ya Bunge hilo, Mbunge huyo
akahojiwa sababu iliyomfanya awe nje ya Jengo wakati zoezi la kura
likiendelea, katika kujitetea akajibu kwamba alijikuta akilazimika
kutoka nje ya kikao kutokana na nguo ya ndani aliyokuwa ameivaa ilikuwa
ikimbana sana hivyo asingeweza kuvumilia kuendelea kukaa ndani ya kikao
hicho.
Pat Martin alijitetea
kwamba anadhani kilichomponza ni kitu ambacho kimewaponza wengi pia
ishu ya kutaka kununua vitu vya bei poa ama kuomba kupunguziwa bei za
vitu.
Yeye alinunua
nguo hizo za ndani nyingi baada ya kuzikuta zikiuzwa kwa nusu bei,
akanunua nyingi bila hata kujua kama zilikuwa zinamtosha size au hapana.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269