Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya akitoa baadhi ya maelekezo kwa
fundi anaejenga geti litakalotumika kutoza ushuru kwa watalii wa nje na
wa ndani watakaofika kuona maporomoko ya mto Kalambo (Kalambo Falls)
ambayo ni maporomoko ya pili kwa ukubwa barani Afrika. Maporomoko hayo
ambayo yapo Mkoani Rukwa mpakani na nchi jirani ya Zambia yamekuwa
yakinufaisha zaidi upande Zambia ambao wamejenga miundombinu kadhaa
kuwawezesha na kuwavutia wanaofika kuona maporomoko hayo. Mto
unaotengeneza maporomoko hayo upo nchini Tanzania na hata muoenekano
mzuri unapatikana kutokea upande wa Tanzania. Kufuatia hali hiyo Mkuu wa
Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya ameamua kusimamia kidete kuhakikisha
miundombinu kadhaa inajengwa katika eneo hilo la maporomoko ili
rasilimali hiyo adimu iweze kutambulilaka na kutoa mchango wa kiuchumi
kwa taifa na Halmashauri husika ya Wilaya ya Kalambo.
Jengo
ambalo litatumika kama geti la kuingilia katika maporomoko ya Mto
Kalambo na ambalo pia litatumika kama eneo la kutoza ushuru kabla ya
watalii kuingia kushuhudia maporomoko hayo likiwa katika hatua ya ujenzi
wa awali.
Afisa Habari Mkoa wa Rukwa Ndugu Hamza Temba akifurahia maajabu ya maporomoko ya Mto Kalambo.
Katibu
wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Ndugu Frank Maten(Kulia) na baadhi ya watalii
wa ndani waliofika kuangalia maporomoko hayo wakifurahia maumbile ya
asili ya eneo hilo.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269