Mahakama
ya Hakimu Mkazi Mkoa ya Njombe, imemhukumu aliyekuwa mkuu wa kituo cha
Polisi Ilembula kifungo cha miaka 30 jela, baada ya kukutwa na hatia ya
kumbaka mtuhumiwa aliyekuwa ndani ya mahabusu.
Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Augustine Rwezile, baada ya mshtakiwa huyo James Nyambenga kukiri
kosa hilo mahakamani, ambapo mshakiwa huyo anadaiwa kumtoa msichana
huyo kwenye chumba cha mahabusu alikokuwa anashikiliwa na kumbaka.
Mwanamke huyo ambae ni mhudumu wa bar alikuwa anashikiliwa kwenye mahabusu ya kituo hicho kwa tuhuma za uzururaji.
Akisoma hukumu hiyo Hakimu Rwezile amesema
ushahidi uliotolewa na upande wa mlalamikaji na vielelezo vya daktari
aliyempima msichana huyo viliweza kuithibitishia Mahakama kuwa mtuhumiwa
alitenda kosa hilo. Chanzo: Gazeti la Nipashe, Feb 20, 2015.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269