Breaking News

Your Ad Spot

Mar 9, 2015

WACHEZAJI HAWA WALIOTEMEANA MATE UWANJANI WAPEWA ADHABU



slapPamoja na kukataa kwamba hakumtemea mate mshambuliaji wa New Castle Papis Cisse, beki wa Man United, Jonny Evans amefungiwa mechi sita na  Shirikisho la soka England FA. Naye Papis Cisse amefungiwa michezo saba na Shirikisho hilo.
FA imetoa adhabu hiyo baada ya kuthibitishwa kupitia mkanda wa video ya mchezo uliochezwa Jumatano iliyopita katika uwanja wa St. James Park ambapo Man U waliibuka na ushindi wa goli 1-0, goli lililofungwa na Ashley Young.
evance
Adhabu hiyo itamfanya beki huyo kukosa mchezo wa robo fainali dhidi ya Arsenal siku ya jumatatu kwmenye uwanja wa Old Tranford na michezo mingine atakayoikosa ni ile dhidi ya Tottenham, Liverpool, Aston Villa, Manchester City, na Chelsea. Kwa upande wa Cisse atakosa michezo dhidi ya Everton, Arsenal, Sunderland, Liverpool, Tottenham,Swansea na Leicester

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages