Mwanasheria
mkuu wa chama cha upinzani nchini CHADEMA, Tundu Lissu leo ametangaza
kuvuliwa uanachama kwa mbunge wa Kigoma Kasikani Zitto Kabwe baada ya
Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam
kutupilia mbali pingamizi la mbunge huyo la kuzuia asijadiliwe.
"Kwa
mujibu wa katiba ya chama cha CHADEMA, mwanachama yoyote anapofungua
kesi mahakamani dhidi ya chama chake, endapo atashindwa katika kesi hiyo
atakuwa amejiondoa uanachama wake, kwahiyo natangaza rasmi rasmi Zitto
Kabwe sio mwanachama tena wa Chadema.
Kwa
upande wake Zitto Kabwe amesema hawakuwa na wito wa mahakamani leo na
Jaji wa kesi kahamishiwa Tabora na hawana taarifa ya Jaji Mpya, pia
kaongeza kuwa Mwanasheria anafuatilia na atatoa statement.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269