Breaking News

Your Ad Spot

Mar 6, 2015

WATU WATANO WANAODAIWA KUWA WACHAWI WAKUZUWIA MVUA WAUAWA KWA KUCHAPWA VIBOKO ,VIONGOZI WA SERIKALINA SUNGU SUNGU WATAJWAKUHUSIKA

Jeshi la polisi mkoa wa Mara limewakamata watu  saba wakiwemo viongozi wawili wa Serikali  ya  kijiji cha Park Nyigoti katika kata ya Ikoma wilayani Serengeti mkoani Mara baada ya kutuhumiwa kuwakamata na kuwafunga vitambaa usoni watu wanane wanaowatuhumu kwa uchawi  kisha kuwachapa viboko na kusababisha vifo vya watu watano. 


Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Mara,kamishina msaidizi  wa jeshi la polisi ACP Ernest Kimola,amesema katika tukio hilo  limesababisha  watu  wengine  watatu kujeruhiwa na viboko hivyo na kulazwa katika hospitali teule ya Nyerere DDH Mjini Mugumu wilayani Serengeti.
 Amesema mbali na mwenyekiti na mtendaji wa serikali ya kijiji kukamatwa pia viongozi wawili wa jadi wamekamatwa wakihusishwa na mauaji hayo.

Amesema kabla  ya kuwakamata wananchi  hao wakiwa katika miji yao  kisha kuwafunga vitambaa usoni na kuwachapa  viboko hadi  kufa  kwa  madai ya  kujihusisha na vitendo vya ushirikina,viongozi hao jadi  kwa kushirikiana na Serikali  ya kijiji waliitisha  mkutano  kwa  lengo la kuwabaini watu wanajihusisha na ushirikiana ambao  umesababisha mvua  kutonyesha  kijijini hapo  ambapo  watu wanane  walitajwa  katika  mkutano  huo.


Kaimu kamanda huyo wa polisi  mkoa  wa Mara,amewataja waliouawa katika tukio hilo lililotokea alfajiri ya tarehe 2.3.2015 kisha miili yao kutupwa karibu na miji yao kuwa ni Nyahita Nyambeho,Nyasari Holela,Joseph Msoba,Nyangi Nyakitambara na Nyangi Kanyaro wote  wakazi  wa kijiji hicho  ambapo Raphael Holela,Masenze Nyamsero na Elizabeth Mwita  wamelazwa katika hospitali ya Nyerere DDH baada ya kuchapwa viboko na kujeruhiwa vibaya.

Hadi sasa jeshi la polisi  kutoka makao  makuu  ya mkoa  wa Mara kwa kushirikaina  na polisi mjini wilayani  Serengeti  wanaendesha na operesheni kali katika kuwasaka watu wote walihusika kufanya mauaji hayo ya kinyama.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages