Breaking News

Your Ad Spot

Jun 1, 2015

MCHUJO SHINDANO LA MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2015 WAANZA LEO JIJINI DAR

 Eluka Kibona, Meneja Utetezi na Ushawishi wa Oxfam akielezea juu ya shindano la Mama shujaa wa Chakula na kumkaribisha Mgeni Rasmi kufungua rasmi hafla ya Maamuzi ya fomu za shindano la Mama shujaa wa Chakula 2015 leo.
 Muwakilishi wa Mgeni Rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa TBS Joseph Masikitiko  katika Hafla ya maamuzi ya fomu za shindano la mamashujaa wa Chakula Bi. Stella E. Mrosso ambaye ni Mkuu wa mahabara ya Chakula TBS akifungua rasmi hafla hiyo ya kuanza kuzihakiki fomu hizo .
 Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster akiwashukuru TBS , Majaji pamoja na washiriki ambao ndio watazipitia fomu hizo kabla hazijafika kwa majaji.
 Mratibu wa Programu kutoka Care International in Tanzania Maureen Kwilasa akisisitiza jambo wakati wa Hafla hiyo
Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster, Mkuu wa maabara chakula TBS Stella E. Mrosso, Tusfaye Legesse Obole President's Delivery Bureau, Manager Agriculture Productivity na  Mratibu wa Programu kutoka Care International in Tanzania Maureen Kwilasa wakiwa katika hafla hiyo.
 Mkuu wa maabara chakula TBS Stella E. Mrosso aliye Mwakilisha Mgeni rasmi katika hafla hiyo akimkabidhi rasmi fomu za shindano la mama shujaa wa chakula  Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster kwa ajili ya kuanza kufanya maamuzi.
Vijana wenye fani mbalimbali  kutoka vyuo vikuu na taasisi mbalimbali  wakiwa katika mchakato kwa kuzipitia Fomu zote za maombi ya kushiriki shindano la mama shujaa wa Chakula 2015
 ******
Na Mwandishi Maalum
Shindano la mama shujaa wa chakula limeingia katika hatua mpya baada ya zoezi la kukusanya fomu za washiriki kutoka mikoa mbalimbali nchini kupitiwa na majaji kwa ajili ya mchujo ambapo washiriki 18 watapatikana kisha baadaye 15 bora ambao wataingia kijijini kwa ajili ya mchakato wa kugombea nafasi ya mama shujaa wa chakula mwaka 2015.

zoezi la kusahihishwa fomu  limezinduliwa mapema leo hii na mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TBS, Joseph Masikitiko ambaye ni Mkuu wa Maabara na Chakula TBS, Bi. Stella Mrosso akiwa sambamba na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Oxfam Tanzania, Jenny Foster na majaji watakaopitia zoezi zima la mchujo wa fomu hizo.

 akizungumza na wageni waandishi wa habari katika uzinduzi huo Mkuu wa Maabara na Chakula, Bi. Stella Mrosso alilisifu shirika la Oxfam kuwa mstari wa mbele katika kupigania haki za wanawake, umiliki wa ardhi na kuhamasisha uzalishaji wa chakula kwa wazalishaji wadogo wadogo.

Bi. Stella alisisitiza kuwa kila mzalishaji anapaswa kuzalisha bidhaa bora ili kushindana na soko la ndani na la nje huku akifafanua kuwa kwa kupitia SIDO, TFDA na Wizara ya Afya, wazalishaji wadogowadogo watakuwa na uwezo wa kupata kibali kutoka TBS bure na kuongeza kuwa wakina mama nchini watumie shindano la mama shujaa wa Chakula kama chachu ya kujitokeza kwa wingi katika mashindano yanayofuata huku wengine wakijifunza uzalishaji bora kupitia mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages