Breaking News

Your Ad Spot

Jul 4, 2015

BRIGHTERMONDAY TANZANIA YATOA FURSA KWA WANAOTAFUTA AJIRA KUWATEMBELEA KWENYE MAONYESHO YA SABASABA

DSC_9352
Meneja Masoko wa kampuni ya Brightermonday Tanzania, Lugendo Khalfan ndani ya hema la banda la Jakaya Kikwete akiwa tayari kukuhudumia wewe mtanzania utakayetembelea banda lao katika viwanja vya maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara ‘Sabasaba’, yanayoendelea kurindima kwenye viwanja vya Mwl. J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.( Picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
Watafuta ajira kote nchini Tanzania wamehamasishwa kujisajili na tovuti ya Brighter monday ili wapate fursa ya kuunganishwa na watoa ajira.
Akifanya mahojiano na mtandao wa habari wa modewjiblog.com, Meneja Masoko wa Brighter monday Tanzania Khalfan Lugendo, amesema usajili huo mbao ni bure, utamwezesha mhusika kupata taarifa mbalimbali na kuweza kuomba nafasi tofauti za kazi ambazo zimewekwa katika tovuti hiyo.
Amesema Brightermonday inajivunia kuwa ndio tovuti namba moja ya ajira nchini Tanzania kwa kuwa idadi ya kazi wanazoziweka katika mtandao huo ni nyingi kuliko chanzo chochote kile cha ajira nchini Tanzania.
Bw. Lugendo ameongeza kuwa kwa mwaka jana 2014 waliweza kuweka nafa za ajira 30,000 na hivyo kuwarahisishia waajiri mchakato mzima wa kuajiri na kupata watu wenye viwango bora zaidi.
Aidha ametoa wito kwa watu wote wanaotembelea maonyesho ya mwaka huu ya kimataifa ya biashara Sabasaba, kutembelea banda lao lililopo katika hema la Jakaya Kikwete ambapo watapata maelekezo kuhusu namna ya kuweza kupata ajira kwa urahisi.
Ametaja namna ya kuwapata ni kupitia anuani ya tovuti ambayo ni www.brightermonday.co.tz au e-mail : info@brightermonday.co.tz,
Simu: +255688 333 334,
Katika mitandao ya kijamii wanapatikana kwa anuani zifuatazo
facebook: brightermondaytz,
Instagram: brightermondaytz pia katika Googleplus na Twitter.
DSC_0109
Key Account Manager wa Brightermonday Tanzania, Gloria Nyiti kwenye sehemu maalum ya kupokea wageni katika banda lao lililopo ndani ya hema la Jakaya Kikwete.
DSC_0310  
Wafanyakazi wa Brightermonday Tanzania wakitoa huduma kwa mmoja wa wateja aliyetembelea banda lao lilipo ndani ya hema la Jakaya Kikwete kwenye maonyesho sabasaba.
DSC_9343
Gloria Nyiti akiwahudumia watafuta ajira katika banda la Brightermonday lililopo ndani ya hema la Jakaya Kikwete.
IMG_6607
Gloria Nyiti akitoa maelekezo ya namna ya kujisajili kwenye mtandao wa Brightermonday kwa mmoja wa wateja aliyetembelea banda lao kwenye maonyesho ya sabasaba yanayoendelea kupamba moto jijini Dar.
DSC_0318  Timu ya wafanyakazi wa Brightermonday Tanzania wakiwa nadhifu katika banda lao tayari kuwahudumia wateja kwenye maonyesho ya Sabasaba.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages