Rais Pierre Nkurunziza
Na RFI
Zoezi la kuhesabu kura limeanza Jumanne jioni wiki hii nchini Burundi baada ya uchaguzi wa urais ambao umesusiwa na upinani na kufutiliwa mbali na jumuiya ya kimataifa.
Rais anaye maliza muda wake Pierre Nkurunzinza anatarajiwa kushinda kwa asilimia kubwa, baada ya kushindana na vyama vidogo vitatu ambavyo ni washirika wa utawala.
Marekani imeonya kuwa uchaguzi uliofanyika Jumanne Julai 21 katika mazingira yanayojiri kwa sasa nchini Burundi hautakuwa wa kuaminika na utazidi kuidhoofisha serikali, amesema John Kirby, msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Marekani.(P.T)
Na RFI
Zoezi la kuhesabu kura limeanza Jumanne jioni wiki hii nchini Burundi baada ya uchaguzi wa urais ambao umesusiwa na upinani na kufutiliwa mbali na jumuiya ya kimataifa.
Rais anaye maliza muda wake Pierre Nkurunzinza anatarajiwa kushinda kwa asilimia kubwa, baada ya kushindana na vyama vidogo vitatu ambavyo ni washirika wa utawala.
Marekani imeonya kuwa uchaguzi uliofanyika Jumanne Julai 21 katika mazingira yanayojiri kwa sasa nchini Burundi hautakuwa wa kuaminika na utazidi kuidhoofisha serikali, amesema John Kirby, msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Marekani.(P.T)
John
Kirby amesema ana hufo kuwa zoezi hilo la uchaguzi lililogubikwa na
utata, huenda liikazua vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Wakati
huo huo Ubelgiji imesema haiutambui uchaguzi huo ambao umefanyika katika
mazingira ya kutatanisha, huku ikibani kwamba haitozitambua taasisi
zitakazotokana na uchaguzi wa urais na ule wa wabunge na madiwani.
Pierre Nkurunzinza anawania awamu ya tatu madarakani, licha ya awamu mbili za kukaa madarakani zilizowekwa kwa mujibu wa katiba.
Wagombea
wengi kupitia vyama vya upinzani wamesusia uchaguzi huo. Wakati huohuo
katika kijiji cha Buye kaskazini mwa nchi, alikozaliwa Rais Nkurunziza
mlolongo wa watu wamejitokeza kupiga kura.
Uchaguzi
huu umefanyika katika hali ya wasiwasi ya kisiasa baada ya kusitishwa
kwa mazungumzo kati ya serikali na upinzani. Kama ilivyokua katika
uchaguzi wa wabunge na madiwani Juni 29, upinzani umeamua kususia
uchaguzi huu.
Marais wa
zamani, Sylvestre Ntibantunganya na Domitien Ndayizeye, ikiwa ni pamoja
na kiongozi wa chama cha Frodebu Nyakuri, Jean Minani, walionesha
msimamo wao, kwamba matokeo ya uchaguzi huo yatakua batili. Lakini kwa
upande wake mwenyekiti wa Tume huru ya Uchaguzi (Ceni), amesema zoezi la
kuondoa faili zao kwenye Tume huru ya Uchaguzi halikufuata utaratibu.
Wangelipaswa kila mmoja kuandika barua yake binafsi ya kuondoa faili zao
kwenye tume huru ya Uchaguzi, amesema Pierre Claver-Ndayicariye.
"
Hatutashiriki katika uchaguzi huu wa kuigiza na tunatoa wito kwa wafuasi
wetu kususia uchaguzi huu ", wamesema viongozi hawa wa kihistoria
katika siasa nchini Burundi.
Hata
hivyo mshauri mkuu wa rais katika masuala ya mawasiliano, Willy Nyamitwe
amesema uamzi wa viongozi hao hauna uzito wowote wakati huu.
" Wakati
wanajua kuwa hawana usemi wala nguvu yoyote wakati huu nchini, ni lazima
watafute kisingizio cha kujiondoa katika uchaguzi ", amesema Willy
Nyamitwe.
Mashambulizi ya guruneti na milio ya risasi
Hayo
yakijiri Jumatatu alaasiri wiki hii utawala wa Bujumbura ulikutana na
mabalozi wa Umoja wa Ulaya, ambapo kulijitokeza mvutano kati ya pande
hizi. Mabalozi wa Umoja wa Ulaya wameitaka serikali kurudi kwenye meza
ya mazungumzo ili kutafutia ufumbuzi mgogoro unaendelea kushuhudiwa
nchini humo. Mabalozi hao wameendelea kusema kuwa kuna hatari nchi ya
Burundi kukumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Wakati huo huo milio
ya risasi na milipuko ya mabomu imeendelea kusikika Jumatatu jioni hadi
usiku kucha mjini Bujumbura, hasa katika wilaya za Bwiza na Nyakabiga.
Inaarifiwa
kuwa watu watatu ikiwa ni pamoja na raia mmoja na askari polisi wawili
wameuawa usiku wa Jumatatu kuamkia Jumanne wiki hii mjini Bujumbura.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269