Breaking News

Your Ad Spot

Jul 11, 2015

URAIS CCM: JK AONGOZA KIKAO CHA NEC LEO KUCHAGUA TATU BORA WATAKAOPELEKWA MKUTANO MKUU

 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwasalimia wajumbe baada ya kuwasili ukumbini kuendesha kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM, leo katika Ukumbi wa jengo la White House mjini Dodoma. Kikao hicho ni cha kuchagua wagombea watatu kati ya watano waliopitishwa na Kikao Cha Kamati Kuu ya CCM kwa ajili ya kuwania kugombea Urais kwa tiketi ya CCM. Watatu watakaopatikana leo, watapelekwa kuigiwa kura katika Mkutano Mkuu wa CCM ili kupata mgombea mmoja atakayepeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi huo mkuu. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) Dk. Ali Mohamed Shein na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa utanguzi kumkaribisha Kikwte kufungua mkutano huo. Kushoto ni Dk. Shein na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akifungua kikao hicho
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiongoza kikao hicho
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete (kushoto_ alipoingia ukumbini. Waliosimama mbele ni Wajumbe waalikwa wa kikao hicho kutoka Baraza la Ushauri la Wazee Marais wastaafu Ali Hassani Mwinyi na Benjamin William Mkapa na wengine ni Makamu Wenyeviti wastaafu Mzee John Malecela na Mzee Pius Msekwa
 Kikao hicho kikiendelea
YALIYOJIRI KABLA YA KIKAO HICHO
 Aliyekuwa muomba kuteuliwa kugombea Urais kwa tiketi ya CCM, ambaye ameenguliwa, Edward Lowassa akiwasili kwenye Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM kuhudhuria kikao cha NEC.
 Lowassa akiingia ukumbini
 Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM wa mikoa, Mzee Msidai akizungumza na waandishi kabla ya kuingia ukumbini kwenye kikao hicho cha NEC
 Mjumbe wa NEC, Dk. Chegeni akizungumza na waandishi kabla ya kuingia ukumbini
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga Hamis Mgeja akizungumza na waandishi kabla ya kuingia ukumbini
 Katibu wa NEC wa Uchumi na Fedha, wa CCM, Zakiah Megji akizungumza na waandishi kabla ya kuingia ukumbini
 Aliyekuwa muomba kuteuliwa na CCM kuwania Urais, Steven Wasira akifuatwa na Waandishi wakati akiingiaukumbini
 Kada wa CCM kutoka Zanzibar, Mohamed Raza akizungumza na waandishi ambapo aliipongeza Kamati Kuu ya CCM kwa kuweza kufanya uteuzi wa watu watano na kueleza kuwa inabidi waliokosa kuteuliwa wawe watulivu kwa kuwa ndiyo Demokrasia
 Muomba kuwania Urais kwa tiketi ya CCM, Bernard Membe ambaye amefanikiwa kuingia tano bora, akizungumza na waandishi kabla ya kuingia ukumbini kwenye kikao hicho leo
 Muomba kuteuliwa kuwania Urais kwa tiketi ya CCM, ambaye ameingia tano bora,  John Magufuli, akimsikiliza kwa makini mmoja wa wajumbe wa NEC, aliyekuwa akimnong'oneza jambo kabla ya kuingia ukumbini
 Waomba kuteuliwa kuwania Urais kwa tiketi ya CCM ambao wamefanikiwa kuingia tano bora, Januari Makamba na John Magufuli wakivheka kwa furaha walipokutana nje ya ukumbi kabla ya kuingia kwenye kikao hicho.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akibadilishana mawazo na Januari Makamba ambaye amefanikiwa kuingia tano bora waliokuwa nje ya ukumbi wakati wa kikao hicho
 Wakuu wa vyombo vya habari vya CCM, Angel Akilimali (Uhuru FM) na Ramadhani Mkoma (Uhuru Publications Ltd
 Muomba ridhaa ya CCM kuwania Urais Bernard Membe akiwasalimia wajumbe ukumbini pengine kuomba kura zao kabla ya kuanza kikao hicho
 Waomba ridhaa ya CCM kuwania Urais, ambao wamefanikiwa kuingia tano bora Bernard Membe na Dk. Asha Rose Migiro wakisalimiana ukumbini wakati wa kikao hicho. Kushoto ni Samwel Sitta ambaye pia aliomba nafasi hiyo lakini hakuingia tano bora
 Aliyekuwa muomba kuteuliwa na CCM kuwania Urais, Lazaro Nyalandu ambaye hakuingia tano bora, akizungumza na Adam Malima
 Wajumbe wakiwa ukumbini
 "Usijai kaka" Katibu wa NEC, Iikadi na Uenezi Nape Nnauye akimfariji aliyekuwa muomba rudhaa ya CCM kuwania Urais, Mwiguku Nchemba, ambaye hakuingia tano bora.
 "Usijai kaka" Katibu wa NEC, Iikadi na Uenezi Nape Nnauye akimfariji aliyekuwa muomba rudhaa ya CCM kuwania Urais, Mwiguku Nchemba, ambaye hakuingia tano bora.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimsalimia Edward Lowassa ambaye hakpita tano bora, wakati wa kikao hicho.
 "Naomba kura yako Ndugu yangu" Bernard Membe ambaye amepitishwa na Kamati Kuu kuingia tano bora akimsalimia Edward Lowassa ambaye amekosa kuingia tano bora, wakati wa kikao hicho.
 "Naomba kura yako Ndugu yangu" Bernard Membe ambaye amepitishwa na Kamati Kuu kuingia tano bora akimsalimia Edward Lowassa ambaye amekosa kuingia tano bora, wakati wa kikao hicho
 "Naomba kura yako Ndugu yangu, tena napiga magoti" Bernard Membe ambaye amepitishwa na Kamati Kuu kuingia tano bora akimsalimia Edward Lowassa ambaye amekosa kuingia tano bora, wakati wa kikao hicho
 January Makamba ambaye amefanikiwa kuingia tano bora akimsalimia Lowassa wakati wa kikao hicho cha NEC
 Membe na Januari Makamba wakisalimiana ukumbini
 Baadhi ya wajumbe ukumbini
 Mwigulu Nchemba akiteta jambo na Mzee Sitta wakati wa kikao hicho cha NEC
 Dk. Asha-Rose Migiro ambaye amefanikiwa kuingia tano bora akimsalimia Lowassa na kumuomba kura wakati wa kikao hicho cha NEC leo
 Baadhi ya wajumbe wa Sekretarieti wakiwa kwenye kikao hicho
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishauriana jambo na Katibu wa NEC, Itikadi na uenezi Nape Nnauye kabla ya kuanza kikao hicho cha NEC
Ulizni ukiwa umeimarishwa katika jengo la White House baada ya baadhi ya walioomba  ridhaa ya CCM kuwania urais na kutoingia tano bora, kudaiwa kuandaa fujo wakati wa kikao hicho cha NEC. Picha zote na Bashir Nkoromo

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages