Breaking News

Your Ad Spot

Sep 20, 2015

BILIONEA DANGOTE AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA KIWANDA CHAKE CHA SARUJI MTWARA


 Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote (aliyesimama katikati), akizungumza na maofisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Mambo y Nje, Viwanda na Biashara na Masoko, Kituo cha Uwekezaji Tanznia (TIC) na taasisi mbalimbali za serikali, walipokutana na Mtendaji huyo mkoani Mtwara jana kujadili kuhusu uzinduzi wa kiwanda hicho kikubwa cha simenti.



 Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote (kushoto), akiwasikiliza kwa makini maofisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje, Viwanda, Biashara na Masoko na Kituo cha Uwekezaji Tanzani (TIC), waliotembelea kiwanda cha simenti cha Dangote kinachojengwa mkoani Mtwara jana kwa ajili ya maandalizi ya kuzindua rasmi Oktoba mwaka huu.

 Mwekezaji kutoka Nigeria, Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote (kushoto), akiwasikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Dangote Makao Makuu, Bw. Sada Ladan Baki (kulia), Mwakilishi Mkazi wa Makampuni hayo, Bi. Esther Baruti na Kaimu Balozi wa Nigeria, Bw. S. Umaru, alipokutana nao kwenye mradi mkubwa wa ujenzi wa kiwanda cha simenti mkoani Mtwara jana.

Bendera zikipepea kwenye kiwanda hicho kikubwa kuliko vyote Afrika Mashariki na Kati

 Sehemu ya mitambo kiwanda hicho ambayho baadhi ujenzi wake umekamilika




No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages