Breaking News

Your Ad Spot

Sep 24, 2015

HEKA HEKA ZA KAMPENI ZA DK MAGUFULI GEITA


 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli (juu kulia) akihutubia katika mkutano wa kampeni kwenye Uwanja wa Karangalala mjini Geita leo. Dk Magufuli  akishinda urais amehidi kuboresha maisha ya wananchi  kwa wachimbaji wadogo wadogo  Geita kuwapatia vitalu vya kuchimba madini pamoja na kuboresha mishahara na marupurupu ya watumishi wa serikali nchini. Pia ameazimia kuanzisha viwanda vidogo vidogo na vikubwa  ili mazao ya wakulima na wafugaji yapande thamani
 Dk Magufuli akiondoka kwenye mkutano huku gari lililombeba likilindwa na vikosi vya ulinzi na usalama mjini Geita leo.
 Dk Magufuli akiwaaga wananchi wa Geita kwenye Uwanja wa Karangalala baada ya mkutano wa kampeni kumalizika
 Dk Magufuli akijinadi kwa wananchi mjini Geita.
 Mfuasi wa CCM akijinasibu kwa kuonesha dole gumba alama ya CCM huku akiwa na jembe na nyundo ambazo ni alama za chama hicho zikimaanisha ni chama cha wakulima na wafanyakazi.
 Wananchi wa Rulenge wilayani Ngara wakimsikiliza kwa makini Dk Magufuli akiwahutubia baada msafara wake kuuzuia ulipokuwa ukielekea wilayani Bukombe, Geita
 Wananchi wa Magamba wakimshangilia Dk Magufuli huku wakiwa na majani  yanayoashiria amani

 Mtoto akiwa na mkungu wa ndizi kichwani huku akisikiliza Dk Magufuli akitoa ahadi kwamba akishinda katika Uchaguzi ujao wanafunzi wa darasa la kwanza hadi kidato cha nne watakuwa wanasoma bure
 Wananchi wakisikiliza kwa makini wakati Dk Magufuli akijinadi wilayani Biharamulo alipokuwa akipita kwenda wilaya ya Bukombe, Geta kuendelea na kampeni
 Mambo yalivyokuwa Nyakanazi, wiayani Biaharamulo
 Mkutano wa kampeni ulivyokuwa Runzewe  wilayani Bukombe

Wauza ndizi wakimpungia mkono Dk Magufuli alipokuwa akienda kwenye mkutano wa kampeni katika Mji mdogo wa Katoro, Jimbo la Busanda, Geita.
Watoto wakifanya jitihada za kumuona Dk Magufuli katika mkutano wa kampeni mjini Katoro leo
Hata juu ya paa waliweza kukaa ili wamsikilize na kumona Dk Magufuli  katika mkutano wa kampeni mjini Katoro
Hadi juu ya mti walikaa
Dk Magufuli akihutubia katika mkutano wa kampeni mjini Geita leo
Mgombea ubunge Geita Vijijini, Joseph Musukuma akishangilia baada ya Dk Magufuli kuahidi ujenzi wa barabara ya Km 10 katika mji wa Geita.
Wananchi wakinyoosha mikono juu kukubali kumpigia kura Dk Magufuli katika uchaguzi mkuu Oktoba 25, mwwaka huu.
Ulinzi ukiwa umeimarishwa  kwenye msafara wa Dk Magufuli mjini Geita.

 Mgombea wa urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuliakiwa jukwaani na wanachama waliohamia CCM.
 Mgombea wa urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwa jukwaani wakati Mwana F.A akitumbuiza kwenye mkutano wa kampeni za CCM mjini Geita.
 Wasanii wa Bongo flava wakipiga push up kumuunga mkono Mgombea wa urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufulikwenye uwanja wa Karangalala.
 Mabango ya Mgombea wa urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli yakiwa yametanda kila kona ya mji wa Geita.


 Mgombea wa urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita Ndugu Joseph Musukuma pamoja na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza Dk. Anthony Diallo kabla ya kuanza kuhutubia wakazi wa mji wa geita waliofurika kwenye uwanja wa Karangalala.
 Burudani kutoka kikundi cha Geita zilivutia sana.

 Yamoto Bendi wakitumbuiza kwenye mkutano wa Mgombea wa urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli,Geita mjini.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages