Breaking News

Your Ad Spot

Sep 26, 2015

MAMA SAMIA ARINDIKA KWA MIKUTANO YA KAMPENI MKOANI MOROGORO LEO

Msafara wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan ukiwasili mkoani Morogoro leo ukitokea mkoani Dodoma.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimsalimia Katibu wa CCM mkoa wa Morgoro Rojas Romuli wakati wa mapokezi yake, alipowasili mkoani Morogoro kufanya mikutano ya kampeni katika mkoa huo leo
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimsalimia mgombea Ubunge Jimbo la  Gairo, Ahmed Shabby wakati alipowasili mkoani Morogoro, kufanya mikutano ya kampeni mkoani humo.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwapungua mkono wananchi waliofika kumlaki alipowasili mkoani Morogoro leo. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa na wapili ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Morogoro, Inocent Karogeresi
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Gairo A, kuhutubia mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro.
Baadhi ya wananchi wakiwa na mabango kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika jimbo la Gairo leo.
Katibu wa CCM, mkoa wa Morogoro, Rojas Romuli akihutubia wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika viwanja vya shule ya msingi Gairo A katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro
Mgombea Ubunge jimbo la Gairo Ahmed Shabiby akihutubia wananchi katika mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika leo katika jimbo hio mkoani Morogoro
Umati wa wananchi ukiwa umefurika kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Gairo A, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro
Mwananchi akionyesha bango la kumfagilia Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro
Mbunge wa Afrika Mashariki, Angela Kizigha akimvalisha kanga za CCM, Bibi Fatuma Farijala, baada ya kuona mavazi yake yamechakaa, akiwa mmoja wa wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro leo
Wananchi wakimshangilia Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassa alipohutubia mkuano wa kampeni leo katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro
Wananchi wakimshangilia Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassa alipohutubia mkuano wa kampeni leo katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimtambulisha aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Gairo, Yona Senyagwa, baada ya kutangaza kuhamia CCM wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Gairo mkoani Morogoro. Kulia ni aliyekuwa Katibu wa zamani wa Chadema kwa miaka kumi John Mwenda ambaye pia alitangaza kuhamia CCM wakati wa mkutano huo
---------------------------------------------------------------------------------------
JIMO LA MIKUMI
 Msafara wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu ukiwa umezuliwa njiani na wananchi katika eneo la Rudewa, wakati akiwa njiani kwenda kuhutubia mkutano wa kampeni leo katika jimbo la Mikumi mkoani Morogoro
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi baada ya kuzuia msafara wake katika eneo la Kilosa mkoani Morogoro leo
 Mkazi wa Kilosa mkoani Morogoro, akiwa amembeba mtoto wake mabegani huku akimsikiliza Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu, baada ya wananchi kuzuia msafara wake katika eneo hilo  leo
 Wananchi wakiwa wamezuia msafara wa mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika eneo la Masanze mkoani Morogoro leo
 Mwananchi akiwa amemkinga jua mtoto aliyembeba mgomgoni huku akimsikiliza Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan alipozungumza na wananchi baada ya kuzia msafara wake katika eneo la  Masanze mkoani Morogoro leo
 Msafara wa Mama Samia ukishangiliwa wakati ukiondoka eneo la Masanze
 Mgombea Mwenza wa Uras kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mwanamuziki wa Kizazi Kipya Juma Kiroboto maarufu kwa jina la Juma Nature, alipowasili kwenye mkutano wa kampeni aliofanya katika jimbo la Kilosa mkoani Morogoro leo.
 Msani wa Bongo Movie, Vincent Kigosi maarufu kwa jina la Ray, akizungumza kwenye mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika leo katika jimbo la Kilosa mkoani Morogoro leo. Ray ambaye awali alikuwa Ukawa, sasa yupo CCM katika kampeni inayoitwa "Nimestuka".
 Wananchi wakishangilia wakati wa mkutano wa kampeni wa Mama samia uliofanyika leo katika jimbo la Kilosa mkoa wa Morogoro
 Msani wa Bongo Movie, Wema Sepetu akimuombea kura mgombea Uras kwa tiketi ya CCM, John Magufuli katika mkutano wa kampeni uliofanyika Jimbo la Kilosa mkoani Morogoro
 Mgombea ubunge jimbo la Kilosa, Jonas Nkya akiomba kura baada ya kunadiwa na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu Hassan wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo hilo.
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Kilosa mkoani Moroogoro.
-------------------------------------
JIMBO LA MVOMELO
 Wananchi wakiwa na mabango ya kumlaki Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan alipowasili kuhutubia mkutano wa kampeni leo katika jimbi la Mvomelo mkoa wa Morogoro
 Mgombea Ubunge jimbo la Mvomelo,  Suleiman Sadik, akiomba kura baada ya kutambulishwa na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa kampeni uliofanyika Mlali katika jimbo hilo leo.
 Mkuu wa wilaya ya Mvomelo, Bety Mkwasa (katikati) akifuatilia kwa makaini hotuba ya Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katikaMlali jimbo la Mvomelo mkoani Morogoro.Kushoo ni Mgmbea Udiwani Jimbo la Mlalo, Frank Mwananziche
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa kiketi ya CCM, Mama samia Suluhu Hassan akimnadi Mgombea Udiwani Kata ya Mlali Frank Mwanaziche katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Mvomelo mkoa wa Morogoro. Kulia ni Mgombea Ubunge jimbo la Mvomelo Sadik Murad
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiagana na Mkuu wa mkoa wa Mvomelo Bety Mkwasa baada ya mkutano wa kampeni uliofanyika leo jimbo la Mvomelo mkoani Morogoro.PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages