Breaking News

Your Ad Spot

Sep 18, 2015

MKUTANO WA KAMPENI YA MGOMBEA WA URAIS CCM DK. ALI MOHAMED SHEIN , JIMBO LA MKOANI PEMBA

Mgombea Urais wa Zanzibar Kupitia CCM Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg Vuai Ali Vuai alipowasili katika viwanja vya mkutano vya Chokocho Wilaya ya Mkoani Pemba kwa ajili ya kampeni yake kwa wananchi wa Jimbo hilo la Mkoani.
Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akiwa na Viongozi wa Siasa jukwaa kuu baada ya kuwasili katikac viwanja hivyo kwa ajili ya mkutano wake wa Kampeni katika viwanja vya mpira Black Wizard Chokocho Wilaya ya Mkoani Pemba.
Wanachama wa CCM wakimshangilia Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, alipowasili katika viwanja vya Mkutano wake wa Kampeni Jimbo la Mkoani Pemba.
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi wakiwa katika viwanja vya mkutano wa Kampeni ya Urais wa Zanzibar kupitia CCM katika viwanja vya Mpira Black Wizard Chokocho Pemba ,
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg Vuai Ali Vuai, akizungumza na Wananchi wa Wilaya Mkoani Jimbo la Mkoani Pemba akiwatambulisha Viongozi waliofuatana na Dk Shein wakati wa Mkutano wake wa Kampeni Pemba.Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Pemba Mkoa wa Kaskazini Pemba Ndg Mberwa Hamad Mberwa akizungumza wakati wa Mkutano huo wa Kampeni ya Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages