Breaking News

Your Ad Spot

Dec 23, 2015

MAGUFULI ASAIDIA VITUO VYA KULEA WAZEE ZAWADI ZA CHRISMAS HUKO ZANZIBAR

Mnikulu wa Ikulu Zanzibar Bw.Ameir Ali Khatib akimkabidhi Mbuzi Sister Mary Gemma wa kituo cha Wazee Welezo, hafla hiyo imefanyika katika makaazi ya Wazee hao Welezo Zanzibar, Vyakula hivyo vimetolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa ajili ya Wazee hao kujumuiika na Wananchi katika kusherehekea Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya. 
Mlukulu wa Ikulu Zanzibar Ndg Ameir Ali Khatib akimkabidhi Mafuta ya Kupikia Sister Mary Gemma wa kituo cha Wazee Welezo, hafla hiyo imefanyika katika makaazi ya Wazee hao Welezo Zanzibar, Vyakula hivyo vimetolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli kwa ajili ya Wazee hao kujumuiika na Wananchi katika kusherehekea Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya. 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uwezeshaji Ustawi wa Jamii Vijana Wanawake na Watoto Zanzibar Ndg. Msham Abdalla akiozungumza wakati wa hafla hiyo ya kukabidha vyakula hivyo vilivyotolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli. 
Wazee wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wakati wa hafla hiyo ya kukabidhiwa Vyakula kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya vilivyotolewa na Rais wa  Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli kwa Wazee hao. kuweza kushiriki kwa vizuri katika sikukuu hizo.
Viongozi wa Kijiji cha Wazee wa Wasiojiweza Welezo Zanzibar wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uwezeshaji Ustawi wa JamiiVijana Wanawake na Watoto Ndg Msham Abdalla wakati wa hafla hiyo ya kukabidhi msaada wa vyakula kwa Wazee wa Welezo Zanzibar.
 Msimamizi wa Kijiji hicho cha Wazee Welezo Zanzibar Sister Mary Gemma akitowa shukrani kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa msaada huo umefika wakati muafa na kutowa shukrani zake kwa Nioba ya Uongozi wa Kituo hicho kinachohudumia Wazee wasiojiweza Zanzibar.
Mzee wa Kijiji cha Wazee Wasiojiweza Welezo Zanzibar Mzee Shein Kombo akitowa shukrani kwa niaba ya Wazee wa Kijiji hicho kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli kwa msaada wake kwa Kuwakumbuka na kumtakia kazi njema katika uongozi wake na kumalizia.
 Hapa Kazi Tu. Imetayarishwa na Othman Mapara.Blogspot  Zanzinews.com

1 comment:

  1. Mungu awabariki ..taifa bado tunaitaji ushirikiani kuwabeba wazee wetu....

    ReplyDelete

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages