Breaking News

Your Ad Spot

Dec 31, 2015

SAMATA AJIUNGA NA KRC GENK, KLABU AMBAYO ILICHEZEWA NA MASTAA HAO MAARUFU

December 30 mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga katika klabu ya TP Mazembe ya Jamuhuri wa kidemokrasia ya Kongo Mbwana Samatta amekiri kuwa katika harakati za mwisho za kwenda kucheza soka barani katika klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji.
Samatta ambaye December 30 alikiri kuwa bado hajasaini na Genk kama inavyoripotiwa ila mambo yanaenda vizuri, kama Samatta akifanikiwa kujiunga na klabu ya KRC Geng ya Ubelgiji, atakuwa katika headlines za wakali kadhaa waliowahi kuichezea timu hiyo na sasa wanatamba katika Ligi kubwa barani Ulaya. Mtu wangu wa nguvu naomba nikusogezee list ya mastaa 4 ambao wamewahi kupitia katika klabu anayokwenda Samatta.
1-  Thibaut Courtois huyu ni golikipa wa Chelsea alijiunga na klabu ya Chelsea mwaka 2011 akitokea klabu ya KRC Genk aliyodumu nayo kuanzia mwaka 2009 hadi 2011 ndio aliamua kutimkia Chelsea.
afp-532661467-e1408807653653
Thibaut Courtois
2- Kevin De Bruyne kwa sasa ni moja kati ya wachezaji waliosajiliwa kwa fedha nyingi kuingia katika klabu ya Man City akitokea Vfl Wolfsburg ya Ujerumani. De Bruyne aliwahi kuchezea klabu ya Genk kuanzia mwaka 2008-2012. Baada ya hapo alijiunga na Chelsea ila mwaka 2014 ndio akauzwa na klabu ya Chelsea kwenda Vfl Wolfsburg.
2BCF932900000578-3216120-The_club_s_record_signing_will_be_expecting_to_become_a_mainstay-a-45_1440951185575
Kevin De Bruyne
3-  Christian Benteke ni staa wa kimataifa wa Ubelgiji mwenye asili ya Kongo. Benteke aliwahi kucheza klabu ya KRC Genk ya kwao Ubelgiji hadi mwaka 2012 klabu ya Aston Villa ya Uingereza ilipoamua kumsajili na mwaka 2015 kumuuza kwenda Liverpool.
1437625706_276577
Christian Benteke
4- Jelle Vossen huyu amecheza Genk kwa muda mrefu zaidi ya wachezaji wengine niliowataja hapo juu, Jelle Vossen amecheza klabu ya KRC Genk kuanzia mwaka 2006 hadi mwaka 2015 ndio aliamua kujiunga na klabu Jelle Club Brugge ya huko huko Ubelgiji, ambayo pia ilishiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu.
Vossen
Jelle Vossen

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages