Breaking News

Your Ad Spot

Dec 29, 2015

WAFANYAKAZI SABA WA BANDARI YA DAR ES SALAAM MBARONI, WENGINE WANANE WATOROKA

 Seehmu ya magari yakiwa kwenye bandari ya Dar es Salaam hivi karibuni
Na K-Vis Media/Khalfan Said
WAFANYAKAZI Saba wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, TPA, Bandari ya Dar es Salaam, wametiwa mbaroni na polisi huku wengine wanane wakitoroka wakituhumiwa kula njama za kuikosesha serikali mapato yatokanayo na kodi na ushuru mwingine, baada ya kubainika upotevu wa makontena elfu 11, 884, na magari 2019.
Waliotiwa mbaroni hadi kufukia asubuhi ya leo Desemba 29, 2015 ni pamoja na       John Elisante, Leticia Masaro,Christina Temu, Marina Chawala,Adnan Ally,Msoud Selemani na Benadeta Sangawe.
Waliotoroka na wanasakwa na polisi ni pamoja na Happy Naftal,Nathan Edward, Aron Lusingu, Amani Kazumari, John Mushi, Valentine Sangawe, Bonaseet Kimaina na Zainab Bwijo.

Upotevu huo umetokea kwenye bandari kavu 7 tofauti ikiwemo ile ya kampuni kubwa hapa nchini, AZAM, ambayo kwa mara nyingine tena imejikuta inaingia kwenye kashfa ya kukwepa kodi baada ya kubainika kuwa makontena 779 kati ya makontena hayo yaliyotajwa hapo juu yalipita bandari ya Dar es Salaam bila kulipiwa ushuru.

Kashfa hiyo imegundulika kufuatia ziara ya kushtukiza aliyofanya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi, na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa mara tu baada ya kuapishwa na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, kushika wadhifa huo.
Waziri Mbarawa amesema pia jumla ya magari 2,019 nayo yameingia nchini bila ya kulipiwa ushuru.

Profesa Mbarawa amesema, kashfa hiyo mpya imebainika baada ya Waziri Mkuu, Mh. Kassim Majaliwa kuagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania, TPA kwa kushirikiana na vyombo vingine wafanye uchunguzi wa kina ili kubaini hujuma dhidi ya mapato ya taifa pale bandarini.

Kufuatia uchunguzi huo, Profesa Mbarawa amesema, makontena na magari hayo baada ya kupitishwa bandarini na kupelekwa kwenye bandari kavu 7 tofauti ndipo yalipoyeyuka yakiacha upotevu wa kodi jumla ya shilingi za Kitanzania Bilioni 49.

Aliyataja makampuni yanayomiliki bandari hizo kavu kuwa ni pamoja na Azam, ambapo makontena 779, bandari kavu ya TRH 4,424, JEFAG, 1450), AMI, 4,384.

Makampuni  mengine ni MOFED makontena 61 na kampuni ya DICD 491,
Waziri Mbarawa amesema baada ya kubaini upotevu hadi kufikia leo  Desemba 29 mwaka huu watumishi 7 kati ya 15 waliokuwa wamehusika na ukusanyaji wa mapato ya Wharfage katika ICD na CFS wamekamatwa na kufikishwa polisi ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria huku wengine wanane wakiwa wametoroka na polisi imeanza kuwasaka.

Waziri Mbarawa ametoa siku 7 makapuni ya uwakala 243 yaliohusika na upotevu huo wawe wamelipa kodi hizo.



 Bandari ya Dar es Salaam, ambayo bado inakumbwa na msuko suko wa uvushaji mizigo bla kulipa kodi
 Waziri Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, (wapili kulia), wakati wa ziara yake ya kushtukiza pale bandarini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages