Breaking News

Your Ad Spot

Jan 31, 2016

SIMBA YAICHAPA AFRICAN SPORTS YA TANGA UWANJA WA TAIFA


MPIRA UMEKWISHAAA 
Dk 90+2, Simba sasa wanatoa shoo tu, ni pasi fupifupi
DAKIKA 3 ZA NYONGEZADk 89, Mgosi anafunga bao zuri kabisa, lakini mwamuzi anasema aliotea. Inaonekana mwamuzi wa akiba hakuwa makini
DK 87, Mgosi aliyeingia punde, anakanyagwa na beki Gereza wa African Sports, lakini mwamuzi anashindwa kutoa adhabu katika tukio hilo
Dk 84, Majegwa na Kessy wanagongeana vizuri lakini shuti la ajib linapanguliwa na kipa wa Sports
KADI Dk 80 Ally Ramadhani wa Sports analambwa kadi ya njano kutokana kucheza kindava
SUB Dk 77 Simba inamtoa Ugando na nafasi yake anachukua Said Ndemla
GOOOOOO Dk 75 Ugando anaifungia Simba bao safi kabisa baada ya Simba kufanya shambulizi la kushitukiza
Dk 73, Ally Ramadhani anapiga shuti, mpira taratibu unagonga mwamba lakini unaokolewa
Dk 70, Uganda anajaribu kuwatoka mabeki wawili wa Sports lakini mpira unashindwa kufika alivyotarajia
Dk 63, Simba wanafanya shambulizi tena lakini Sports wanakuwa makini na kuokoa
Dk 57, krosi nzuri ya Ramadhani inaokolewa na Isihaka na Simba wanaondosha hatari.
Dk 56, Bado Simba wanaonekana kuwa vizuri zaidi wakitawala mchezo katika kiungo
Dk 51, Ajibu anamlamba chenga beki mmoja ana kuachia shuti kali, kipa Zacharia Maarufu anadaka, anautema lakini anauwahi
Dk 46, Simba wanaanza kwa kasi utafikiri wanatakiwa kusawazisha lakini Sports wanaonekana pia bado wako vizuri
MAPUMZIKO
Inaonekana Simba wametawala mpira kwa 58% dhidi ya 42% ya Sports. Hivyo ni kipindi bora zaidi kwa upande wa Simba
Dk 44 hadi 45, Simba ndiyo wanaonekana kumiliki mpira zaidi na presha kubwa kwa African Sports
GOOOOOO Dk 43, Kiiza anawachambua mabeki wa African Sports na kufunga bao safi kabisa 
Dk 35 hadi 40, Simba wanendelea kumiliki mpira kwa kupiga pasi fupifupi
Dk 34, Ajib anawatoka mabeki wa Sports lakini anachelewa na mpira wake unaishia mikononi mwa kipa wa Sports
GOOOOOOO Dk 31, Kessy anafanya kazi nzuri na kufunga bao zuri kabisa la pili kwa mchezo wa leo
Dk 28 hadi 30, Simba wanaendelea kuumiliki mpira kwa pasi fupifupi huku wakipiga krosi ndefu na fupi na African Sports wanaendelea kucheza pasi ndefu
Dk 27, Simba wanagongena vizuri, Ajib anatoa pasi nzuri ya Kisigino kwa Kiiza, lakini shuti lake linapita nje ya lango
Dk 24, Kessy anawachambua walinzi wawili wa African Sports, hata hivyo mwamuzi anasema Kiiza alikuwa ameishaotea
Dk 16  hadi 19, Simba wanaonekana kuongeza mashambulizi na kuwapa presha kubwa Sports huku Kazimoto anaonekana kuwa mwiba zaidi kwa viungo wa Sports
GOOOO Dk 14, krosi nzuri kabisa ya Kessy inatua kwa Kiiza anamalizia vizuri na kuandika bao kwa Simba
Dk Dk 5 hadi 8, mpira zaidi unachezwa katikati ya uwanja na hakuna timu iliyofanya shambulizi kali
Dk 2 hadi 4, Simba wanaendelea kutawala katika, KAzimoto, Mkude wakiendelea kugongeana vizuri na kuwapa wapinzani wao wakati mgumu
Dk 1, mpira unaanza taratibu, Simba wanaonekana kupiga pasi nyingi katikati, lakini African Sports pia wanaonyesha utulivu
#(Kwa hisani ya Saleh Jembe Blog)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages