Breaking News

Your Ad Spot

Jan 31, 2016

WACHINA WAISHIO NCHINI TANZANIA WAADHIMISHA MWAKA MPYA 2016 “NGEDERE”

np1
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye akifungua Mwaka Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam. Kushoto ni mshereheshaji aliyejitambulisha kwa jina la “Sharobaro”.
np2
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye (kushoto) akibadilishana mawazo na Waziri Mkuu Mtaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Salim Ahmed Salim (kulia) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya wa Kichina wa 2016 unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
np3
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye (kulia) akifuatilia michezo mbalimbali wakati wa wa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mshauri wa Mambo ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania Gao Wei.
np4
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye (katikati) akifuatilia michezo mbalimbali wakati wa wa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam. Kulia ni Waziri Mkuu Mtaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Salim Ahmed Salim na kushoto ni Mshauri wa Mambo ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania Gao Wei.
np5
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye (kushoto) akisalimiana na Waziri Mkuu Mtaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda (kulia) alipowasili viwanja vya Mnazi Mmoja wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere”
np7
Baadhi ya wageni waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016
np8
np9 np11
Baadhi ya raia wa Kichina wakiendelea na kujipamba kabla ya kuanza kwa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016
np12 np14
Baadhi ya michezo iliyooneshwa wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere”
np15 np16
Waziri Mkuu Mtaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda akichanganya tiketi za bahatinasibu wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mwaka Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere”
np17
Vimulimuli vy fataki zilizowashwa kuashiria kuzinduliwa kwa Mwaka Mpya Kichina wa 2016 unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo mwishoni mwa wiki viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)

………………………………………………………………………………………………
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Jumuiya ya Wachina wanaoishi nchini wamezindua na kuukaribisha kwa shamrashamra mwaka Mpya wa 2016 unaojulikana kama mwaka wa “Ngedere” kulingana na utamaduni wa nchi hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.
Akizindua shamrashamra hizo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye alisema kuwa Wachina na Watanzania ni ndugu ambao uhusiano wao ni wa kudumishwa milele na milele.
“Uhusiano wa Tanzania na China ni wa kihistoria ambao ni wa muda mrefu katika mambo mbalimbali ikiwamo kijamii, kiuchumi, kisiasa, kielimu na kiutamaduni Utamaduni na kimawasiliano kati ya nchi hizi mbili” alisema Waziri Nape.
Kihistoria, uhusiano wa China na Tanzania ni wa kidugu na kirafiki wakati wote iwe wa dhiki au faraja katika maisha ya kila siku kati ya Watanzania na Wachina.
Ni wakati muafaka kuongeza jitihada za kuimarisha uhusiano na ushirikiano wan chi hizo mbili ili kuwaenzi waasisi wa ushirikiano huo ambao ni Rais Mwalimu Julius Nyerere  na Mao Tse Tung.
Kwa upande wake Mshauri wa Mambo ya Utamaduni kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania Gao Wei alisema kuwa wanajisikia faraja wakati wote wanapofanya kazi na Watanzania kwa kuwa wanamengi ya kujivunia katika historia ya nchi hizo.
Aidha, shamrashamra za mwaka mpya wa Kichina zilihudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo Mawaziri Wakuu Wastaafu Salum Ahmed Salum, Mizengo Pinda, viongozi mbalimbali na wenyeji wa sherehe hizo ambao ni raia wa Kichina wanaoishi nchini wakiongozwa na viongozi kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania.
Mwaka huu unajulikana kama “Ngedere” wakati mwaka 2015 ulijuklikana kama “Kondoo” ambapo maadhimisho ya Mwaka Mpya wa “Ngedere” yalipambwa na michezo mblimbali ikiwemo bahatinasibu, sarakasi, nyimbo, muziki wa ala, mazingaombwe na ngoma.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages