Breaking News

Your Ad Spot

May 6, 2016

WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO KUTOA TAARIFA YA VIFO VYA UZAZI KILA ROBO MWAKA

um1
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na Wajumbe wa Mkutano wa Viongozi Wanawake katika masuala ya Afya katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam 5 Mei, 2016.
um2 um4
Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mhe. Einar Hebogard Jensen akiongea na Wajumbe wa Mkutano wa Viongozi Wanawake katika masuala ya Afya katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam, 5 Mei, 2016.
um5
Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mhe. Einar Hebogard Jensen akiongea na Wajumbe wa Mkutano wa Viongozi Wanawake katika masuala ya Afya katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam, 5 Mei, 2016.
um6
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) pamoja na Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mhe. Einar Hebogard Jensen wakifurahia burudai toka kwa Vijana wakiotumbuiza stejini (hawapo pichani) wkaati wa Mkutano wa Viongozi Wanawake katika masuala ya Afya uliofanyika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam 5 Mei, 2016.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO.
………………………………………………………………………………………………………………………….
Na Jonas Kamaleki- MAELEZO.
 
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inakusudia kutoa taarifa ya wanawake wanaofariki Dunia kutokana na matatizo ya uzazi kila baada ya miezi mitatu ili kukabiliana na tatizo la vifo vya wanawake nchini.
 
Hayo yamesemwa na Waziri wa  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu leo jijini Dar es Salaam wakati akifungua Mkutano wa Viongozi Wanawake katika masuala ya Afya.
 
“Nimeamua kuhakikisha wanawake wanapiga hatua na kuthaminiwa katika jamii, na nimeamua kuanza kutoa ripoti ya robo mwaka kwa kila Halmashauri kuhusu taarifa ya wanawake wanaofariki kutokana na matatizo ya uzazi,” alisema Ummy Mwalimu.
 
Ameeleza kuwa, katika uteuzi atakaoufanya kwenye bodi zilizo chini ya Wizara yake, atahakikisha asilimia 30 ya wajumbe wa bodi hizo ni wanawake. Baadhi ya Bodi zilizo chini ya Wizara yake ni pamoja MSD, TFDA na Bodi ya Wafamasia.
 
Aidha, Mhe. Ummy amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutekeleza sera ya elimu bure ambapo amesema wazazi watalazimika kuwapeleka watoto wa kike shuleni kwa wingi kuliko ilivyokuwa awali.
 
Katika kutilia mkazo suala la elimu kwa wasichana, Waziri Ummy amasema watoto wa kike hawana budi kujitambua na kuzingatia masomo ambayo ndiyo yatawafanya waweze kuchagulika au kuteuliwa kushika nyadhifa kubwa za uongozi. “Hamsini kwa Hamsini bila elimu ni siasa tu” alisisitiza Mhe. Waziri.
 
Mhe. Ummy amewataka wanawake kujituma katika kufanya kazi ili kuibadilisha jamii. Hapa akaja na kauli mbiu kuwa “Mwanamke akitenda, jamii itatenda, Tanzania Itasonga mbele’’.
 
Kwa upande wake Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Bibi Fatuma Mrisho amewasisitiza watoto wa kike kuthamini masomo na kuepuka ndoa za utotoni. Amesema kuwa mtoto anapokuwa shuleni anaepuka Ukimwi kwa asilimia saba. Hivyo amesema ni lazima wasichana kupenda shule na kuacha kurubuniwa na wavulana.
 
Huu ni mkutano wa utangulizi kabla ya mkutano Mkubwa wa karne kuhusu Afya, Haki na Ustawi wa Wasichana na wanawake ambao wajumbe zaidi ya 5,000 wakiwemo viongozi wa Dunia, Wasomi, Watunga sera, Wanaharakati, Watu wa habari, dini, Vyama vya kijamii na Wawakilishi wa sekta binafsi watashiriki.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages