Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wazee wa Ruangwa ambao
walimshukuru kwa jitihada kubwa anazofanya za kuboresha maisha ya
Wanachi wa jimbo lake la uchaguzi. Alikuwa katika ziara ya jimbo lake
la uchaguzi Julai 16, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wazee wa Ruangwa ambao
walimshukuru kwa jitihada kubwa anazofanya za kuboresha maisha ya
Wanachi wa jimbo lake la uchaguzi. Alikuwa katika ziara ya jimbo lake
la uchaguzi Julai 16, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wananchi Ruangwa kabla ya kuhutubia
mkutano wa hadhara kwenye uwanja uliopo kwenye kata ya Nachingwea
mjini Ruangwa Julai 16, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akimpongeza Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Lindi ,
Renather Mzinga ambaye amepandishwa cheo na kuwa Kamishina Msaidizi
Mwandamizi wa Polisi. Alikuwa katika ziara ya mkoa wa Lindi Julai
16,2016.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi, viongozi na baadhi ya
wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo
Julai 16, 2016. Kulia ni Mkuu wa Mkoa huo, Halima Dendego na wapili
kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
Baadhi
ya Watumishi , Viongozi na wananchi wa mkoa wa Mtwara wakimsikiliza
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa
Mkuu wa Mkoa huo Julai 16, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi
ya Watumishi , Viongozi na wananchi wa mkoa wa Mtwara wakimsikiliza
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa
Mkuu wa Mkoa huo Julai 16, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
……………………………………………………………………………………………….
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amesema uamuzi wa Serikali wa kufuta tozo tano
kati ya tisa alizokuwa anakatwa mkulima wa zao la korosho uko pale pale
na unatarajiwa kuanza kutumika katika msimu mwaka huu hivyo ameitaka
Bodi ya Korosho kusimamia uamuzi huo.
“Watendaji
wa Serikali katika ngazi mbalimbali mnatakiwa kuhakikisha kwamba
maelekezo haya yanafuatwa. Malengo yetu ni kumpunguzia mkulima mzigo wa
tozo nyingi alizokuwa anakatwa,” alisema.
Waziri
Mkuu ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumamosi, Julai 16, 2016) wakati
akipokea taarifa ya maendeleo ya mkoa Mtwara pamoja na taarifa ya
kuondolewa kwa baadhi ya tozo katika zao la korosho zilizowasilishwa na
Mkuu wa Mkoa huo, Halima Dendego.
Alisema
Serikali iliamua kuzifuta tozo hizo baada ya kubainika kuwa zilikuwa
zikiwanyonya wakulima hali iliyosababisha wauchukie mfumo wa stakabadhi
ghalani.
“Kuanzia
mwaka huu Serikali imeamua mfanyabiashara yeyote wa korosho hana budi
kuanza kulipa malipo ya awali kabla ya kuingia kwenye mnada ili tuwe na
uhakika wa kununua korosho hizo na kuwalipa wakulima kwa wakati,”
alisema.
Akizungumzia
kuhusu changamoto ya kushuka kwa uzalishaji wa korosho Waziri Mkuu
aliutaka mfuko wa wakfu wa kuendeleza zao hilo ufanye utafiti wa kubaini
sababu ili waweze kutafuta namna ya kuipatia ufumbuzi.
“Nitakuja
kukutana na viongozi wa mfuko waniambie wanafanya nini na wamefanya
nini miaka mitatu iliyopita na wana mpango gani huko mbele tunakokwenda
kama hakuna mpango tutauangalia mara mbili mbili kwani wana fedha nyingi
lakini hata mbegu hawapeleki kwa wakulima,” alisema.
Katika
hatua nyingine Waziri Mkuu aliitaka Bodi ya Korosho kuhakikisha kila
msimu wakulima wanapata pembejeo bora na zinawafikia kwa wakati ili
waweze kupata mazao ya kutosha.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269