Breaking News

Your Ad Spot

Aug 30, 2016

MWANDISHI WA HABARI, NDUGU KIVAMWO AHITAJI MSAADA WA KUONGEZWA DAMU

Bw. Simon Kivamwo
Waandishi wa habariwakitoa damu ili kuwezesha matibabu ya Mwandishi wa habari mkongwe hapa nchini Bw. Simon Kivamwo ambaye anapatiwa matibabu kwenye hospitali ya Ocean Raod iliyoko jijini Dar es Salaam leo Agosti 30, 2016.

Kwa mujibu wa Mwandishi wa Habari anayeratibu zoezi hilo Bw.Thompson, Kivamwo ambaye anaugua kwa muda mrefu sasa, amezidiwa na maradhi leo hii na kupelekwa haraka kwenye hospitali hiyo ambapo madaktari walihitaji kumuongezea damu.

 Benjamin Thomspon ametoa  mwito kwa wanahabari na jamii kwa ujumla kujitokeza kumchangia damu mwandishi huyu ili kuokoa maisha yake. Sehemu ya kutolea damu ni Hospitali ya Mnazi Mmoja, Kariakoo jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages