Breaking News

Your Ad Spot

Sep 9, 2016

KOREA KASKAZINI YLIPUA BOMU LA NYUKLIA ‘SAWA NA LA HIROSHIMA’

Mtangazaji wa TV ya Korea akitangaza habari za jaribio hilo
Mtangazaji wa TV ya Korea akitangaza habari za jaribio hilo
Shirika la habari la serikali ya Korea Kaskazini limesema taifa hilo limefanya majaribio ya bomu kupima uwezo wa bomu lake la nyuklia la kurushwa kwa kombora hatua ambayo imeshutumiwa vikali na jamii ya kimataifa.
Mlipuko wa bomu hilo umesababisha tetemeko la ardhi katika eneo lililofanyiwa majaribio.
Tetemeko hilo lilikuwa na nguvu ya 5.3 kwenye vipimo vya Richter.
Maafisa wa jeshi la Korea Kusini wanakadiria kwamba mlipuko huo ulikuwa sawa na wa kilo tani kumi za TNT, ukubwa sawa na wa bomu lililoangushwa Hiroshima na Marekani wakati wa vita vikuu vya pili vya dunia. Baadhi wanasema huenda bomu hilo la Korea Kaskazini likawa lilikuwa na nguvu ya kilo tani 20.
Bomu lililoangushwa Hiroshima mwaka 1945 lilikuwa na nguvu ya kilo tani 15 (tani 15,000).
Bomu lenye nguvu zaidi la nyuklia lililowahi kulipuliwa lilikuwa lile lililopewa jina Tsar-bomba, ambalo lililipuliwa na Urusi mwaka 1961.
Korea
Korea Kaskazini imesea jaribio hilo limefanikiwa
Lilikuwa na nguvu ya mega tani 50, sawa na nguvu ya tani milioni 50 za TNT (50,000,000).
Wataalamu bado wanaendelea kudadisi iwapo lilikuwa bomu la haidrojeni, jambo ambalo linaweza kulipa nguvu zaidi kushinda mlipuko wa bomu la kawaida la nyuklia.
Korea Kaskazini yarusha makombora tenaUN yatishia kuichukulia hatua Korea Kaskazini
Mwanamke maarufu zaidi Korea Kaskazini
Hilo likithibitishwa, basi itakuwa ni mara ya tano kwa Pyongyang kutekeleza jaribio la silaha za kinyuklia.
Jaribio la leo limetekelezwa siku ambayo serikali inaadhimisha kuanzishwa kwa taifa la sasa la Korea Kaskazini mwaka 1948.
Jamii ya kimataifa imeghadhabishwa na hatua hiyo ya Korea Kaskazini.
Rais Kim Jong-un ameonyeshwa kwenye runinga akiwa amejaa tabasamu
Rais Kim Jong-un ameonyeshwa kwenye runinga akiwa amejaa tabasamu
Rais wa Korea Kusini Park Geun-hye ametaja jaribio hilo kuwa "jaribio la kujiangamiza" ambalo linaonyesha "kutomakinika" kwa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un.
Bi Park, ambaye amesitisha ghafla ziara yake ng'ambo, amesema baada ya kutekeleza jaribio hilo la tano la nyuklia "serikali ya Kim Jong-un itakaribisha vikwazo zaidi na kutengwa zaidi na jamii ya kimataifa."
Korea Kaskazini yafanya 'jaribio kubwa la nyuklia'
"Uchokozi kama huu utaongeza kazi safari yake ya kuelekea kwenye maangamizi."
Bi Park alifanya pia amzungumzo ya dharura na Rais wa Marekani Barack Obama kwa njia ya simu.
Kuvumiliwa
China, mshirika mkuu wa Korea Kaskazini kidiplomasia, pia imeshutumu hatua hiyo na kuihimiza Pyongyang kukoma kuchukua hatua ambazo zinaweza kuzidisha hali.
Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe, amesema majaribio kama hayo ya Korea Kaskazini hayawezi kuvumiliwa.
Bw Shinzo Abe.
Bw Shinzo Abe. Japan imeilalamikia Korea Kaskazini
Lakini mwandishi wa BBC anayeangazia Korea anasema wapinzani wa Pyongyang wanatatizika kuhusu ni hatua gani wanafaa kuuchukulia utawala wa Korea Kaskazini.
Tayari waliwekea taifa hilo vikwazo Januari baada ya Pyongyang kufanya jaribio la nne ya nyuklia. BBC

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages