Breaking News

Your Ad Spot

Sep 24, 2016

WAASTAAFU WA JESHI LA MAGEREZA WAAGWA JIJINI DAR

Wastaafu wa Jeshi la Magereza wakiwasili katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji, Ukonga, Dar es Salaam wakiwa wameongozwa na Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile wakielekea Jukwaa Kuu kupokea Salaam ya Heshima. Hafla ya kuwaaga wastaafu wa Jeshi la Magereza imefanyika leo Septemba 23, 2016.
Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile akiwa katika Jukwaa Kuu akipokea Salaam ya Heshima kutoka kwenye Gwaride Maalum la kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza.
Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile akikagua Gwaride Maalum la kuwaaga Wastafu wa Jeshi la Magereza lililoandaliwa na Maofisa wa Jeshi la Magereza.
Gwaride M aalum likipita mbele ya Jukwaa kwa Heshima.
Viongozi Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakipiga Saluti wakati Gwaride Maalum likipita mbele ya Jukwaa kwa heshima. Wa kwanza kulia ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa.
Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile akiwa pamoja na Wastaafu wengine wa Jeshi la Magereza wakitoa Salaam za mwisho wakiwa kwenye magari wakati Gwaride Maalum likiwa limeunda Umbo la OMEGA.
Maofisa na Askari wa Jeshi la Magereza wakipunga mikono ikiwa ni ishara ya kuwaaga Wastaafu hao wakati wakipita katika magari Maalum (hawapo pichani).
Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile akipita kwenye gari Maalum akipunga mkono ikiwa ni ishara ya kuwaaga Watumishi wa Jeshi la Magereza baada ya kustaafu rasmi Utumishi wa Umma kwa mujibu wa Sheria.
Kamishna Mstaafu wa Magereza Deonice Chamulesile(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wastaafu wa Jeshi la Magereza pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages