Breaking News

Your Ad Spot

Oct 8, 2016

OFISI YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI YATOA ZAWADI KWA WANAFUNZI NA WALIMU BORA WA KEMIA NA BAIOLOJIA KITAIFA

02
Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele (kulia), akitoa hotuba wakati wa hafla ya utoaji zawadi kwa wanafunzi na walimu Bora wa masomo ya Kemia na Baiolojia kwa kidato cha Nne na kidato Tano 2014/2015 iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali.
01
Mgeni Rasmi, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bw. Michael John (kulia) akitoa hotuba kabla ya kukabidhi zawadi kwa Wanafunzi na Walimu Bora wa masomo ya Kemia kwa Kidato cha Nne waliomaliza mwaka 2014 na cha Sita 2015. Jumla ya wanafunzi Ishirini na Nne (24) na walimu wane (4) walifanikiwa kupewa zawadi kwenye hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ofisi za Mkemia Mkuu wa Serikali, Jijini Dar es Salaam.
03
Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Serikali, Dkt. Jim Yonazi (kulia) akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wazazi wa wanafunzi waliopata zawadi kwa kufanya vizuri kwenye masomo ya Kemia na Baiolojia kwa Kidato cha Nne 2014 na Kidato cha Tano 2015. Dkt Yonazi alimsindikiza kijana wake Yonazi Charles Senkondo kwenye hafla hiyo
6
 Mwanafunzi Bora wa masomo ya Kemia na Baiolojia kwa upande wa wasichana wa kidato cha sita mwaka 2015, Meghna Solanki (kulia) akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wanafunzi wenzake baada ya kupatiwa zawadi zao.
07
 Wanafunzi Bora wa masomo ya Kemia na Baiolojia kwa Kidato cha Nne na Tano kwa mwaka 2014/2015 wakitambulishwa wakati wa hafla ya kuwapa zawadi iliyofanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Jijini Dar es Salaam.
08
Mgeni Rasmi, Bw. Michael John, akimkabidhi zawadi mwanafunzi, Yonazi Charles Senkondo (kulia) baada ya kuwa mwanafunzi bora kwenye masomo mawili ya Kemia na Baiolojia kwa kidato cha Sita mwaka 2015.
09
 Mgeni Rasmi, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bw. Michael John (wa pili kulia) akimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi Jinai na Huduma za Vinasaba vya Binadamu, Bi. Gloria Omari (kushoto) akieleza shughuli mbalimbali zinazofanywa na Idara hiyo. Wengine kutoka kulia ni Mjumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Esther Lugwisha na Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele (wa tatu kulia). Mgeni Rasmi alikuwa akimuwakilisha Naibu Waziri, Mhe. Hamisi Kigwangalla kwenye Tuzo kwa wanafunzi na walimu Bora wa masomo ya Kemia na Baiolojia kwa Kidato cha Nne 2014 na cha Sita 2015.
010
Mgeni Rasmi, Bw. Michael John (aliyekaa katikati) akiwa pamoja na  Mjumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala, Profesa Esther Lugwisha (wa pili kushoto), Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele (wa pili kulia), Menejimenti ya Wakala, wageni waalikwa, walimu na wanafunzi mara baada ya kumaliza zoezi la utoaji zawadi kwa wanafunzi na walimu Bora wa somo la Kemia na Baiolojia kwa Kidato cha Nne 2014 na Kidato cha Sita 2015 (P.T)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages