Ajali ya lori la mafuta yaua watu wasiopungua 25 nchini Kenya
Mripuko wa lori lililobeba shehena ya mafuta katika barabara moja kuu nchini Kenya umeua watu wasiopungua 25.
Ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia leo eneo la kilomita 10
kaskazini mwa mji wa Naivasha ulioko katika mkoa wa Bonde la Ufa
katikati mwa Kenya.
Akizungumza kutoka eneo la tukio, afisa wa Shirika la Kimataifa la
Msalaba Mwekundu Felister Kioko amesema: "Hadi sasa tumekusanya maiti 25
kutoka eneo la tukio la ajali baada ya lori lililokuwa likielekea
Uganda kupoteza udhibiti na kugonga magari mengine kadhaa."
Itakumbukwa kuwa mwaka 2009 zaidi ya watu 100 waliungua hadi kufa
karibu na mji wa Molo ulioko katikakati mwa Kenya pia baada ya lori
lililobeba shehena ya mafuta ya petroli kuwaka moto.../
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269