Breaking News

Your Ad Spot

Jan 29, 2017

SERIKALI IMESEMA INAFANYA JUHUDI ZA KUOKOA WATU 14 WALIOFUKIWA GEITA

KAL1
Naibu waziri wa Nishati na madini Dr,Merdadi Kalemani akiwasilia katika mgodiwa wa RZ ambako kumetokea tukio la watu 14 kufukiwa na udongo wakati wakiendelea na kazi za uchimbaji.
KAL3
Mbunge wa Jimbo la Busanda ,Lorencia Bukwimba akielekea  kwenye eneo la shimo ambapo watu wamefunikwa.
KAL4
Mbunge wa Jimbo la Busanda ,Lorencia Bukwimba akiwapa pole ndugu na jamaa ambao walikuja kujua kile ambacho kitaendelea kwa undugu zao.
KAL6
Wananchi wakiwa nje ya Ngome ya mgodi wakifatilia kile ambacho kinaendelea
KAL8
Sehemu ambayo inatumiwa kutolea udongo.
KAL9
Ndugu wakiwa katika masikitiko makubwa wakijiuliza ni lini ndugu zao watatoka shimoni.
KAL10
Mkuu wa Mkoa wa Geita  Meja jenerali Ezekiel Kyunga akiwa katika eneo la tukio akifatilia kile kinachoendelea
KAL11
Mkuu wa wilaya ya Geita,Herman Kapufi akipandisha juu baada ya kutoka shimoni
KAL12
KAL14
Naibu waziri wa nishati na madini,Dr Medadi Kalemani akioneshwa baadhi ya maeneo yaliyopata dosari kwenye mgodi huo

NA MADUKA ONLINE
NAIBU waziri wa Nishati na Madini Dk. Medard Kalemani ametembelea Mgodi wa RZ uliofukia Watanzania 13 na raia mmoja wa Nchini China anayetambulika kwa jina la Meng Juping na kusema kuwa serikali itaendelea kuweka nguvu ili kusaidia uokoaji.

Katika ziara yake hiyo ya dharura Naibu Waziri huyo ametoa pole kwa niaba ya serikali kwa uongozi wa Mkoa, Wananchi pamoja na....
Mgodi huo kukumbwa na tukio hilo.

Mara baada ya kupokea taarifa ya maafa hayo, iliyosomwa na kamishina msaidizi wa madini kanda ya ziwa victoria, Dk. Kalemani aliutaka uongozi wa Mkoa pamoja kamati ya uokoaji kujikita zaidi kwenye shughuli ya uokojai na waachane na mambo mengine ambayo yanaweza yakasababisha zoezi hilo liwe gumu.

‘’Ndugu zangu mimi kwa niaba ya serikali kuu napenda nitoe pole kwa hiki kilichowakumba Mkoa pamoja na Mgodi lakini napenda kuwaambia kuwa Kamati ya ulinzi na Usalama pamoja natimu ya uokoaji mhakikishe mnasimamia vyema zoezi hili ili tuwaokoe ndugu zetu ambao wamo humo ndani ya shimo,’’alisema Naibu waziri Kaleman.

‘’Kingine niagize hapa hakikisheni mnatoboa shimo kwa kutumia drilling ili tupate mwanya wa kuwapatia chakula ndugu zetu ambao wamefukiwa na udongo wakati juhudi za kufukua zikiendelea ,’’aliongeza.

Akizungumza na Maduka online mapema asubuhi ya leo  kamishina msaidizi wa madini kanda ya ziwa victoria Yahaya Samamba alisema kuwa kamati ya uokozi kwa kushirikiana kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Geita, ilibadilisha mfumo wa uokoaji kwa kutumia wachimbaji wadogowadogo baada ya mashine za kisasa kufikia usawa mita 20 ambazo haziwezi kuhimili uzito.

‘’Mitambo hii imekomea mita 20 tumeona tutumie wachimbaji wadogo ili twende sambaba na uokoaji uliosalama..kwahiyo usiku wa jana (juzi) saa 5:00 kamili usiku tulisitisha kutumia mashie yaani Magreda kutokana na usawa tuliofikia kuwa laini,’’alisema Samamba.

Kwa upande wake Mhandisi kutoka kampuni ya  uchimbaji ya Busolwa Mine Eng. Nayompa wakati akitoa mtazamo wake namna zoezi hilo linavyokuwa gumu alisema ramani zinazotolewa na wachina ni za kubahatisha na hawana uhakika nazo ndizo sababu zimechelewesha uokoaji na zoezi kuonekana halikamiliki kwa wepesi.

“Mimi ninachokiona hapa wachina hawa ndugu zetu wachina wameshindwa kutupatia ramani ya uhakika ndiyo maana tunabahatisha bahatisha tu..mwandishi hata wewe jana ulikuwa shuhuda namna gari la kutoboa lilivyoshindwa kulenga kwenye shimo  walipo ndugu zetu,’’alisema Eng. Nayompa.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Busandwa ambako tukio hilo limetokea Lolensia Bukwimba alisema haipaswi watu kunyosheana kidole kwa sasa wakati nguvu na jtighada zikiendelea kufanywa.

Hata hivyo Rais wa shirikisho wa vyama vya wachimbaji wa madini ,John Wambura Bina,amepongeza juhudi ambazo zinafanyika kwa makapuni ya madini kujitolea pamoja na serikali na wanaamini kuwa juhudi za uokoaji zinazoendelea zinaweza kuzaa matunda.

Viongozi mbalimbali wa serikali na chama jana walitembelea eneo la Mawemeru kuliko mgodi wa RZ ambao unamilikiwa na wawekezaji wa Kichina huku leseni ya madini ikiwa ni ya Mtanzania Ahamed Mbaraka.

Matumaini kwa siku ya leo yanaonekana kwani hadi kufikia majira ya saa moja kamili watu ambao wapo chini waligonga bomba kwa kuashiria kuwa wapo karibu na sehemu ya kutokea.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages