Breaking News

Your Ad Spot

Mar 16, 2017

AJALI YA LORI LAUA MTU MMOJA MAKETE

Na Edwin Moshi wa Eddy Blog
Lori lililokuwa limebeba mawe limepinduka katika kijiji cha Masisiwe wilayani Makete na kusababisha kifo cha mtu mmoja ambaye alikuwa katika lori hilo.

Taarifa za awali kutoka eneo la tukio zinasema kuwa lori hilo limepoteza muelekeo ghafla kisha likaanza kupinduka kwa kubiringika mara kadhaa umbali unaokadiriwa kuwa zaidi ya mita 80 kutoka barabarani. Ajali hiyo inadaiwa kutokea kati ya saa nane na saa tisa alasiri hii jana.

Baadhi ya mashuhuda waliokuwa eneo la tukio ambao hawakutaka kutaja majina yao wamesema Lori hilo lilikuwa linatoka kubeba mawe kwa ajili ya kujenga daraja katika kata ya Ipepo kabla ya kupoteza mwelekeo likiwa njiani na kupinduka kisha kuporomokea bondeni.
Jeshi la polisi Makete limefika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu kwa uchunguzi zaidi. Tutawaletea taarifa kamili ya tukio hilo pindi mamlaka husika zitakapatia.

Polisi wakipima jinsi ajali hiyo ilivyotokea 
 Askari Polisi akiangalia mawe yaliyokuwa yamebebwa na lori hilo kabla ya kutokea ajali





Mwili wa marehemu ukiingizwa kwenye gari
Mwili wa marehemu ukiwa ndani ya gari la polisi
Lori hilo likionekana kwa mbali baada ya ajali


Muonekano wa lori hilo baada ya ajali




Ajali ilipoanzia, hapa ndipo lori hilo lilipotumbukia

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages