Breaking News

Your Ad Spot

Mar 29, 2017

WADAIWA SUGU NA TANESCO WAONJA JOTO YA JIWE MKOAN KIGOMA

Na Rhoda Ezekiel Kigoma.

SHIRIKA la umeme Tanzania TANESCO Mkoani Kigoma imesitisha huduma za umeme kwa Mamlaka ya Maji safi na Mazingira KUWASA, kufuatia deni la umeme la shilingi bilioni 1.3 ambalo halijalipwa tangu mwaka 2013 hadi sasa hali inayopelekea kukosekana kwa Maji Manispaa ya Kigoma na kupelekea dumu moja la maji kuuzwa shilingi 1000.

Akizungumza na Globu ya Jamii, Kaimu Mkurugenzi wa KUWASA, Muhandisi Mbike Jones alisema Mamlaka ya Maji ilikatiwa umeme wiki iliyopita kufuatia deni lililokuwa linadaiwa tangu mwaka 2013 na limeshindwa kulipwa kutokana na Mamlaka hiyo kutegemea fedha hizo kulipwa na Wizara ya maji.

Jones alisema KUWASA ilijitahidi kufanya mazungumzo na TANESCO waweze kurudisha umeme na kudai kuwa ni maelekezo kutoka Makao makuu, mpaka sasa Wizara imejitahidi kufanya mzungumzo na Wizara ya fedha na kudai kuwa watalitatua tatizo hilo baada ya mazungumzo na Shirika la umeme waweze kulipa kidogo kidogo.

Alisema Mpaka sasa KUWASA inadai taasisi za serikali milioni 380 na Wananchi milioni 330, hali inayopelekea kukwamisha zoezi la ulipwaji wa deni hilo kushindwa kulipwa, na aliwaomba Wananchi na Taasisi zinazo daiwa kulipia madeni hayo ili maji yaweze kurudishwa na kuepukana na kero hiyo.

" niwaombe wananchi wawe wavumilivu na waendelee kuchemsha maji wanayo yachota kwenye vyanzo vya maji, ili kuepukana na magonjwa ya milipuko na wawe wavumilivu jitihada zinaemdelea za kuhakikisha tatizo hilo linakwisha na kuendelea kupata maji kama mwanzoni", alisema Jones.

Nao Baadhi ya Wakazi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji , Athumani Rashidi na Destina Paulo walisema kumekuwa na tatizo la maji hali inayopelekea Dumu moja la maji kuuzwa shilingi 1000 hali niyopelekea Wananchi wenye kipato kidogo kushindwa kumudu gharama hizo na kushindwa kununua.

Paulo alisema kwasasa wanalazimika kwenda kuchota maji kwenye mito na Visima vilivyoko mbali na mji kilomita nane kutokea Mjini hali hiyo inawapelekea kushindwa kukabiliana na kero hiyo, na waliiomba serikali na mamlaka inayo husika kuliahughurikia suala hilo ilikuepukana na kero hiyo.


Baadhi ya wakazi kutoka maeneo mbalimbali wakichota maji kwenye vyanzo vya maji vinavyopatikana mjini humo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages