Breaking News

Your Ad Spot

Mar 1, 2017

WAZAZI TUIUNGE MKONO SERIKALI KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA

 Katibu wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Stanley Mkandawile akizungumza na baadhi ya viongozi wa Jumuia hiyo kutoka katika Kata mbalimbali za wilaya ya Ilala, alipokutana nao katika kikao maalum cha kujitambulisha kwao, kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Ilala. Kulia ni Katibu wa Jumuia hiyo wilaya ya Ilala, Lugano Mwafongo. Akizungumza kwenye kikao hicho, pamoja na mambo mbalimbali Mkandawile ameitaka Jumuia ya Wazazi katika mkoa wake na maeneo mengine nchini, kuunga mkono hatua ya serikali kuingia katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya.
Mkandawile amesema, Kama sehemu ya Wanana CCM, Jumuia hiyo haiba budi kuunga mkono mabambano hayo kwa kuwa Serikali inatekeleza ilani ya CCM, ibaraya 118 hadi 119.
Katibu wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Stanley Mkandawile akiwasili ukumbini. Kushoto ni Katibu wa Jumuia hiyo wilaya ya Ilala, Lugano Mwafongo na kulia ni Katibu wa Jimbo la Ilala Christopher Lugemalila.
 Wajumbe wakiwa ukumbini
Wajumbe wakishangilia jambo ukumbini
Katibu wa CCM Jimbo la Ilala, Said Dogo akitoa maneno ya utangulizi kabla ya kikao kuanza. Kulia ni Mkandawile na Lugano Mwafongo
Wajumbe ukumbini wakifuatilia mazungumzo katika kikao hicho
Mjumbe akiwa kwenye kikao hicho cha Jumuia ya Wazazi huku akiendelea na malezi ya mwanae ukumbini
Mwenyekiti wa CCM, Jimbo la Ilala Christopher Lugemalila akizungumza wakati wa kikao hicho
Katibu wa Jumuia ya Wazazi wilaya ya Ilala, akizungumza wakati wa kikao hicho
Katibu wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Stanley Mkandawile akizungumza na baadhi ya viongozi wa Jumuia hiyo kutoka katika Kata mbalimbali za wilaya ya Ilala, alipokutana nao katika kikao maalum cha kujitambulisha kwao, kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Ilala.
Wajumbe wakimsikiliza Mkandawile
Wajumbe wakimsikiliza Mkandawile wakati akizungumza na watendaji na viongozi wa Jumuia ya Wazazi Wilaya ya Ilala. Picha zote na Bashir Nkoromo

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages