Breaking News

Your Ad Spot

Apr 2, 2017

WANANCHI KUJITOLEA KUKARABATI BARABARA YAO MBAGALA

 Wananchi kwa kushirikiana na madereva kuikarabati Barabara itokayo Mbagala Rangi tatu kwenda kwa Mponda kpitia Vigozi kwa Kashikashi iliyoharibiwa na mvua zinazo endelea kunyesha na kusababisha adha ya usafiri Dar es Salaam leo.  (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)

Na Khamisi Mussa,
Mwananchi aishiye eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina la Athumani Saidi (a.k.a John teli),  aliseama kero yake ni kuhusu Barabara ni mbovu kupitika na adha wanaipata na kuomba wahusika kufanyika kazi kero hizi na anahitaji kujua barabara ipo katika Halmashauri au Manispaa? , na aliseama  Athumani toka kuhamia maeneo hayo anamiaka minne na hajahama na gari lake kutokana na njia mbovu. akimalizia kusema anaiomba Serikali kuwatembelea na kusikia kero zao, na mzee Yusufu Ramadhani Nyanza mkazi wa eneo hilo alikuwa na haya yakusema alisema.

Kubwa ni Daraja ambapo mvua ikinyesha hakuna wa kuvuka mto mzinga na kunawanafunzi hushindwa hata kwenda shule kutokana na  maji kujaa mto huo na panaumbali wa kilometa kumi na tano hadi kufika shule ya Msingi Mianzini. alisema mzee Ramadhani, 

Hospitali hatuna na Kituo cha Polisi kipo Kongowe Mwisho  hivyo  aliomba huduma za polisi na hospitali wasogezewe karibu, tunakuwa kama watu tuliyosahaulika na wananchi wanazidi kuhamia,  alizidi kuiomba serikali kusikia kilio chao





No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages