Basi
la Shirika la Mabasi yaendayo haraka Dar es Salaam (UDART) likitoka
eneo la Hospitali ya Taifa Muhimbili baada ya kuchukua Abiria Mei 10,
2017. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
Abiria wakiingia katika Basi hilo
Baadhi ya Abiria wakiwa katika mstari kuingia katika Gari eneo la Muhimbili ambapo safari imeanza Mei 10, 2017
Baadhi ya Abiria wakipata huduma ya tiketi.
Na Khamisi Mussa.
Safari
tuliyoianzisha ya Muhimbili , tumeianzisha mahususi kwa kuwapunguzia
Abiria wetu Gharama za nauli walizokuwa wakizitumia hapo awali ambapo
walikuwa wakitoka Mbezi na kuja hadi Faya na kupanda Gari jingine.
Hayo
yamesemwa na Meneja huduma, Pius Ragero wakati alipokuwa akizungumza na
waandishi (pichani hawapo) mara baada ya kuanza safari hiyo eneo la
Muhimbili, alianza kwa kusema.
Tumeanzsha safari hiyo la kuwapunguzia abiria wetu gharama za nauli ambapo hapo awali .
Abiria
ilikuwa anatoka, mfano akianzia Mbezi anakuja hadi Faya nakuchukua
usafiri mwingine kuja Muhimbili, sasa atatoka Kimara kwa Sh. 650 hadi
faya na atapanda gari letu litokalo Gerezani
kuja Muhimbili kwa gharama hiyohiyo.
Akianzia
Kivukoni anakuja hadi faya na anapanda gari lakutokea gerezani hadi
Muhimbili na akitokea Morocco anakuja hadi faya na anapanda gari la
kutoka gerezani na kufika Muhimbili.
Hayo yalisemwa na Meneja Huduma, Ragero ambapo alisema, anawaomba abiria kutowa ushirikiano na kupenda huduma yetu kwani tumejipanga kikamilifu, alisema Ragero
Kwa
sasa naona mapungufu hakuna na kama tiketi mtu anafika kituoni na
kupata tiketi na kupanda gari letu na kuanza safari yakuelekea atakako
ilimuradi abiria huyo asitoke nje ya kituo chetu.
Naye abiria aliyefika kupata huduma ya tiketi, Grece Kivugo alisema.
Anashukuru
kwa wahusika julali na kuamua kuanzisha safari hii ya Muhimbili na
kuona umuhimu na kutujali, ila anaomba ifahamike Hospitali ya Taifa
Muhimbili ni hospitali kubwa , inapaswa barabara zinazo ingilia
Muhimbili ziboreshwe na usafi ufanyike kuanzia nje,
Naye
mkazi wa Tandika Juma Adam alikuwa na haya ya kusema, usafiri huu ni
mzuri na bado matatizo madogo madogo bado yapo, kama unavyoona, mtu
anakaa foleni unaambiwa tiketi hakuna kutokana na muitikiwa wa watu
kuupokea usafifiri huo nakuona ni mkombozi kwao, alisema Adam,
Sasa
inatakiwa waboreshe usafiri wawe inatakiwa vituvyote viwe vimekamilika
na inakuwa haina haja ya mtu kuhangaika kwa usafiri na kutozunguushana
na tutakuwatumepata usafiri wa uhakika.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269