Breaking News

Your Ad Spot

May 2, 2017

RAIS DK MAGUFULI AMALIZA ZIARA MKOA WA KILIMANJARO, AREJEA DAR

Moshi, Kilimanjaro
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, leo tarehe 02 Mei 2017, amemaliza ziara ya siku tatu mkoani Kilimanjaro, ambapo akiwa mkoani humo pamoja na mambo mengine alikuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani - Mei Mosi.

Taarifa iliyotolewa na Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Jaffar Haniu, imesema, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Kilimanjaro - KIA, Rais Magufuli ameagwa na viongozi mbalimbali wa mkoa huo wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Saidicky na na Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa.

Raais Dk John Magufuli akiwaaga wananchi baada ya kupata Ndege kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) tayari kujerea Dar es Salaam, leo

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages