Breaking News

Your Ad Spot

May 28, 2017

RAIS DK. MAGUFULI AMTEUA SIMON SIRRO KUWA MKUU MPYA WA JESHI LA POLISI NCHINI

Ikulu, Dar es Salaam.
Rais Dk. John Magufuli leo tarehe Mei 28, 2017 amemteua aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi Simon Sirro kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP).

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Habari, Ikulu jijini Dar es Salaam, Gerson Msigwa  imesema, Sirro anachukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Jeshi hilo, IGP Ernest Mangu ambaye kwa mujibu wa taarifa hiyi atapangiwa kazi nyingine.

Katika taarifa hiyo ambayo Kururugenzi ya Mawasilino ya Rais Ikulu, ameipokea  kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa IGP Simon Sirro ataapishwa kesho Jumatatu Mei 29, 2017 saa 3:30 asubuhi Ikulu Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages