Breaking News

Your Ad Spot

Oct 26, 2017

WAGOMBEA WA UDIWANI WA CCM SARANGA NA KIJICHI, WAREJESHA FOMU KWA KISHINDO DAR, LEO

 Wagombea Udiwani wa CCM katika Uchaguzi wa marudio katika Kata ya Saranga Wilayani Ubungo na Kata ya Kijichi wilayani Temeke leo wamerudisha fomu zao kwa wasimamizi wa uchaguzi katika kata hizo kwa kishondo huku wakisindikizwa na viongozi kadhaa ya wa CCM wakiongozwa ana Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Saad Kusilawe. Pichani, Mgombea wa CCM katika Kata Saranga, Manispaa ya Ubungo Haroun Mdoe akimkabidhi fomu yake Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa Kata hiyo Dandasi Kijo kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji kata ya Saranga, leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Saad Kusilawe na kulia ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ubungo Lucas Mgonja.
 Waendesha bodaboda wakiwa kwenye msafara kumsindikiza mgombea Udiwani kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi wa marudio Kata ya Saranga, leo
 Mashabiki wa CCM wakiwa kwenye bajaji kwenye msafara kumsindikiza mgombea Udiwani kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi wa marudio Kata ya Saranga, leo
 Masafara wa baadhi ya viongozi wa CCM wakipeleka mgombea wa CCM kurejesha fomu kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji Kata ya Saranga  
 Mwananchi aliyekuwa katika shughuli zake akishangilia msafaya wa mgombea huyo wa CCM wa Udiwani Kata ya Saranga
 Shamrashamra za wana CCM zikihanikiza baada ya msafara wa mgombea wa CCM wa Udiwani Kata ya Saranga kufika kwenye Ofisi za Afisa Mtendaji wa wakata hiyo
 Mgombea Udiwani wa CCM katika uchaguzi wa marudio Kata ya Saranga Haroun Mdoe (mwenye fulana yenye jina kubwa la Samia) akishangiliwa wakati akiwasili kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji Kata ya saranga kurejesha fomu yake.
 Wanachi na wana CCM wakimsindikiza kuingia kwenye Ofisi mgombea huyo
 Mgombea wa CCM katika Kata Saranga, Manispaa ya Ubungo Haroun Mdoe akikabidhiwa fomu za kiapo na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa Kata hiyo Dandasi Kijo, kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji kata ya Saranga, leo, huku Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Saad Kusilawe (kulia) Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ubungo Lucas Mgonja (kushoto) wakishuhudia.
 Msimamizi huyo msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Saranga akitazama kama Mgombea huyo wa CCM anajaza fomu yake kwa usahihi. Kulia ni Kusilawe. 
 Mgombea wa CCM akiijaza fomu yake ya kiapo
 Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ubungo Lucas Mgonja akimwelekeza mgombea wa CCM ili asikosee wakati wa kujaza fomu yake ya kiapo 
 Mgombea wa CCM katika Kata Saranga, Manispaa ya Ubungo Haroun Mdoe akimkabidhi fomu yake Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa Kata hiyo Dandasi Kijo kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji kata ya Saranga, leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Saad Kusilawe na kulia ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ubungo Lucas Mgonja.
 Mgombea huyo wa CCM akiwa katika picha ya pamoja na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi kata ya Saranga (wapili kushoto) na baadhi ya viongozi wa CCM baada ya kukabidhi fomu yake ya kuomba kuteuliwa kugombea
 Baadaye mgombea huyo akapiga picha ya pamoja na viongozi wa CCM waliosindikiza na baadhi ya wana CCM waliofika kwenye Ofisi ya Ofisa Mtendaji wa Kata ya Saranga kushuhudia akirejesha fomu. 
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam saad Kusilawe akimpongeza Mgombea Udiwani wa CCM katika Uchaguzi wa marudio Kata ya Saranga Haroun Mdoe baada ya urejeshaji fomu kukamilika. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Kata ya Ubungo Lucas Mgonja na kulia ni Katibu wa CCM Wilaya ya Ubungo Salum Kalli.
 ---------------------
  UREJESHAJI FOMU KATA YA KIJICHI
 Mgombea CCM katika uchaguzi wa marudio Kata ya Kijichi Eliasa Mtarawanje akishangiliwa na wananchi wakati wakiwapungia mkono alipokuwa akienda kurejesha fomu kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji Kata ya Kijichi, Temeke Dar es Salaam, leo.
 Eliasa Mtarawanje akipunga mkono kuonyesha furaha yake ya kwenda kurejesha fomu
 Mwananchi akimshangilia Eliasa Mtarawanje msafara ulipopita eneo la makazi yake.
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Saad Kusilawe na baadhi ya viongozi wa CCM wakimsubiri kumpokea Mgombea huyo Eliasa Mtarawanje, kwenye ofisi ya Afisa Mtendaji kaya ya Kijichi.
 Eliasa Mtarawanje akisalimia viongozi wa CCM baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji Kata ya Kijichi kurejesha fomu yake.
 Eliasa Mtarawanje aakisimama wakati wa utambulisho
 Katibu wa CCM mkoa wa Sar es Salaam Saad Kusilawe akizungumza kwa niaba ya msafara baada ya kufika katika Ofisi ya Afisa Mtedaji Kata ya Kijichi
 Mgombea wa CCM katika Uchaguzi wa marudio wa Udiwani Kata ya Kijichi Eliasa Mtarawanje akikabidhiwa fomu ya kiapo ili kuijaza kabla ya kukabidhi fomu zake.
 Eliasa Mtarawanje akijaza kwa makini fomu yake ya kiapo
 Eliasa Mtarawanje akikabidhi fomu zake kwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi kata ya Kijichi baada ya kuzijaza
 Akikabidhi rasmi fomu hizo baada ya kuhakikiwa 
 Eliasa Mtarawanje Akisaini kuthibitisha kuwa amerejesha fomu zake
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, saad Kusilawe na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Temeke Ndugu Mishi wakimsindikiza kutoka katika Ofisi ya Afisa Mtendaji baada ya kujeresha fomu
Eliasa Mtarawanje akitoka kwa shangwe na nderemo kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji Kata ya Kijichi baada ya kurejesha fomu zake za kuomba kuteuliwa kuwa mgombea wa Udiwani wa kata hiyo kwa tiketi ya CCM. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages