Breaking News

Your Ad Spot

Dec 2, 2017

WAZIRI MHAGAMA AZINDUA MPANGO WA KUWASAIDIA WALEMAVU WENYE THAMANI YA DOLA LAKI 5 SAWA NA SH. BILIONI 1.1 KUTOKA SERIKALI YA KUWEIT

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama (katikati) akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa mbalimbali vya watu wenye ulemavu katika Chuo Cha Ufundi Cha Yombo kinachotoa mafunzo kwa Walemavu, Dar es Salaam jana , kulia ni Balozi wa Kuweit nchini Tanzania,  Jasem Al-Najem.
  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akizungumza jambo mara alipowasili katika chuo hicho
 
  Balozi wa Kuwait nchini,  Jasem Al-Najem akizungumza jambo na  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama (wa kwanza kushoto), wakati mmoja wa mwanafunzi wa Chuo hicho, Lenah Sauli alipokua akishona nguo

 Mkufunzi Mkuu Msaidizi  Regina Makotha (kulia) akizungumza kwa kuwapa ishara yale aliyokuwa akizungumza Waziri Mhagama
 Wanafunzi wa Chuo Cha Ufundi Cha Yombo kinachotoa mafunzo kwa Walemavu wakiashiria kupiga makofi wakati walipokuwa wakipewa ishara na Mwalimu wao, Mkufunzi Mkuu Msaidizi  Regina Makotha (pichani hayupo) Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama alipokuwa akizungumza nao
 Balozi wa Kuweit nchini Tanzania,  Jasem Al-Najem akizungumza jambo katika hafla fupi ya kumkabidhi,  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama (wa pili kushoto) vifaa mbalimbali kwa watu wenye ulemavu ikiwa ni msaada kutoka serikali ya Kuweit, hafla iliyofanyika jana  katika Chuo Cha Ufundi Cha Yombo kinachotoa mafunzo kwa Walemavu, Dar es Salaam jana, wakwanza kushoto ni Katibu Muhutasi wa Balozi na wakwanza kulia ni Mkalimani wa Balozi, Abdallah Yahaya


 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akimkabidhi cherehani, Lenah Sauli (kushoto)

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akimvisha miwani mwanafunzi wa Chuo hicho, Mandela Lamwai ambaye anasomea ufundi umeme
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akimkabidhi mafuta maalumu ya kujipaka kwa watu wenye ulemavu wa ngozi mwanafunzi wa Chuo hicho, Mandela Lamwai ambaye anasomea ufundi umeme, wa tatu kushoto ni  Balozi wa Kuwait nchini Jasem Al-Najem 









KUWAIT YAZINDUA MPANGO KAMILI WA KUWASAIDIA WALEMAVU TANZANIA
Serikali ya Kuwait kwa kupitia Ubalozi wake nchini umezindua mpango kamili wa kuwasaidia watu wenye ulemavu katika Chuo Cha Ufundi Yombo,uzinduzi ambao ulihudhuriwa na Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,vijana,Ajira na Walemavu Mhe. Jenista Mhagama,Kaimu wa Chuo Bi Maryam, walimu na wanafunzi wa chuo hiko kilichoanzishwa mwaka 1973 na kutoa mafunzo mbalimbali kama umeme,ushonaji n.k.
Balozi wa Kuwait Al-Najem katika hotuba yake wakati wa uzinduzi amesema kuwa mpango huo utagharimu kiasi cha dola laki 5 sawa na shilingi bilioni 1.1 utaendeshwa nchi nzima kwa awamu kwa kushirikiana na maafisa wa Serikali ya Tanzania na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali.
Pembezoni mwa uzinduzi huo uliokwenda sambamba na maadhimisho ya siku ya  watu wenye ulemavu duniani, Al-Najem alimkabidhi Waziri Mhagama vifaa vya walemavu kama viti vya matairi,fimbo,magongo,miwani,vifaa vya kuwasaidia wenye udhaifu wa kusikia na mafuta ya kujipaka kwa walemavu wa ngozi albino huku akiahidi kuchangia vifaa ya upasuaji kwa watoto wenye vichwa vikubwa katika Taasisi ya Mifupa MOI.
Kwa upande wake Waziri mwenye dhamana Mhe. MHAGAMA amesema kuwa Tanzania itaendelea kutekeleza maazimio ya kimataifa kuhusu walemavu huku akiyataka mashirika yasiyokuwa ya kiserikali na sekta binafsi kuiga mfano wa Serikali ya Kuwait, watu wake na Ubalozi wake katika kuwasaidia walemavu nchini.
Waziri Mhagama ameishukuru Serikali ya Kuwait kwa misaada hii na kuuomba Ubalozi kusaidia katika kutatua baadhi ya changamoto zinazokabili Chuo cha Ufundi Yombo kama vile uchimbaji wa kisima na makazi kwa wanafunzi walemavu.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages