Breaking News

Your Ad Spot

Feb 4, 2018

NAIBU WAZIRI WA MADINI BITEKO ATATUA MGOGORO WA LESENI YA MADINI ULIODUMU KWA MIAKA KUMI SHINYANGA

Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akihutubia mamia ya wachimbaji wadogo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mwazimba, Kata ya Chela, Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga, Jana Februari 3, 2018
Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akikagua maeneo ya uchimbaji baada ya mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mwazimba, Kata ya Chela, Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga, Jana 3 Februari 2018
Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akikagua maeneo ya wachimbaji wadogo wa chama cha ushirika cha Kasi Mpya Gold Mine katika Kijiji cha Mwazimba, Kata ya Chela, Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga, Jana 3 Februari 2018
Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akihutubia mamia ya wachimbaji wadogo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mwazimba, Kata ya Chela, Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga, Jana 3 Februari 2018.
Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akikagua maeneo ya wachimbaji wadogo wa chama cha ushirika cha Kasi Mpya Gold Mine katika Kijiji cha Mwazimba, Kata ya Chela, Wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga, Jana 3 Februari 2018

Na Mathias Canal, Shinyanga

Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko ametatua mgogoro wa leseni uliodumu kwa takribani miaka kumi kwa kuamuru kupitia haraka eneo la leseni ya uchimbaji wa madini kwa wachimbaji wadogo wa chama cha ushirika cha Kasi Mpya Gold Mine.

Mhe Biteko ametoa agizo hilo Jana 3 Februari 2018 wakati akihutubia mamia ya wachimbaji wadogo waliohudhuria kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mwazimba, Kata ya Chela, Wilayani Kahama kufuatia malalamiko ya Mbunge wa Jimbo la Msalala Mhe Ezekiel Maige sambamba na malalamiko ya wachimbaji wadogo waliyoyawasilisha Wizara ya Madini Mjini Dodoma Januari 26, 2018.

Alisema kuwa wananchi walifunga safari mpaka ofisi za madini kwa ajili ya kupata uhalali wa kupimiwa eneo lao kwa kutumia GPS lakini Kaimu Afisa madini mkazi Wilaya ya Kahama akawabadilishia Nukta (Coordinator) ambazo baadaye zilionekana kuwa za eneo jingine ambalo ni mbuga isiyokuwa na madini huku eneo hilo likihamishiwa kwa ntu mwingine.

Mhe Biteko amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya madini Prof Simion Msanjila kumchukulia hatua za haraka za kinidhamu aliyekuwa Kaimu Afisa madini mkazi Wilaya ya Kahama aliyehusika na upotoshaji wa leseni na kuzua mgogoro wa usumbufu usiokuwa na sababu dhidi ya wananchi na serikali.

Alisema kuwa hakuna sababu ya Wizara ya Madini kukumbatia mgogoro huo wa leseni uliodumu kwa miaka kumi kwa sababu ya eneo ambalo lilipotoshwa na baadhi ya watendaji wa Wizara ya madini kwani jukumu la serikali ni kuwatumikia wananchi ikiwemo utatuzi wa kadhia mbalimbali zinazowakabili katika jamii.

Mhe Biteko kwa msisitizo mkubwa amewataka wachimbaji wadogo kuwa waaminifu na kufichua baadhi ya wachimbaji wanaoficha madini kwa kutorosha bila kulipa kodi kwani kufanya hivyo itakuwa njia pekee ya kuisaidia serikali na kuinusuru katika mtego wa wizi wa rasilimali hizo.

Ameongeza kuwa serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli haitawafumbia macho wamiliki wa leseni hizo ambao leseni zao zimedumu kwa muda mrefu bila kuzifanyia kazi kwani hawazalishi ajira yoyote wala kulipa kodi Hivyo serikali imekusudia kuzifuta na kuwapa watu wengine ambao watazifanyia kazi haraka iwezekanavyo ili kuongeza tija kwa sekta ya madini katika uchangiaji wa pato la Taifa.

Akitoa mfano katika eneo la Kahama kuna leseni 249 lakini zinazofanyiwa kazi ni 18 tu huku wenye leseni zisizofanya kazi wakisubiri wachimbaji wadogo wavumbue madini kisha huja kuwaondoa kwa kisingizio cha umiliki wa leseni. Leseni hizo zikiwa zimedumu kwa muda mrefu bila kuendelezwa.

Aidha,  alisema kuwa kuna maeneo makubwa manne ambayo yameshaamuliwa na serikali kutengwa kwa ajili ya wachimbaji wadogo ikiwemo eneo la Nyang'wale lenye hekari 996, eneo la Nyangarata lenye hekari 1074, Eneo la Buzwagi kilometa za mraba 53.4 na eneo la Kinamyuba kilomita za mraba 33.3

Alisema kuwa jukumu la serikali ni kutatua kero za wananchi sio kuwaongezea kero wananchi hivyo watendaji wote wa serikali wanapaswa kutimiza ndoto ya Rais Magufuli kwa kuwatumikia wananchi kwa imani na matendo imara kwa kuwanufaisha watumishi na rasilimali zao.

Sambamba na hayo Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko amewataka wananchi kuendelea na uchimbaji wakati taratibu zikifuatwa kukamilisha kumaliza mgogoro huo huku akiwahakikishia kutoondolewa tena na endapo kama watakuwa wanahitaji maeneo mengine yaliyotengwa kwa ajili ya wachimbaji wadogo wanapaswa kufuata taratibu za kisheria zilizoainishwa.

Awali mbunge wa Msalala Mhe. Ezekiel Maige alimweleza Mhe. Naibu Waziri kuwa watu wake wameonewa kwa muda mrefu na yeye akifuatilia mgogoro huo bila mafanikio.

"Ni kwasababu ya serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Magufuli kwa kimbilio la wanyonge, mheshimiwa Naibu Waziri nilikua nimekata tamaa" Alikaririwa Mhe Maige aliyekuwa akizungumza kwa hisia huku akishangiliwa na mamia ya wachimbaji wadogo waliokisanyika kwenye mkutano huo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages