Breaking News

Your Ad Spot

Feb 26, 2018

VIDEO : MNEC SALIM ASAS ATOA MSAADA WA MILIONI TANO KWA JUMUHIYA YA WAZAZI KILOLO

Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa, ambae pia ni Mnec wa Mkoa wa wa Iringa Salim Asas akimkabidhi Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Kilolo, kiasi cha shilingi milioni 5 kwa ajili ya ujenzi wa ukumbi wa UWT wilayani humo.


Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taiga ( NEC), Salim Asas akikabidhi kiasi cha shilingi milioni 5 mwenyekiti wa UWT wilaya ya Kilolo kwa ajili ya ujenzi wa ukumbi wa UWT
Asas akipongezwa kwa mchango wake 



Na Fredy Mgunda,Kilolo

MJUMBE wa
halmashauri kuu ya CCM Taifa anayewakilisha Mkoa wa Iringa, Salim Asas ameichangia
jumuiya ya wanawake wa chama cha mapinduzi ( UWT) wilaya ya Kilolo kiasi cha
shilingi milioni 5 kwa ajili ya ujenzi wa ukumbi wa kisasa wa mikutano ya hadhara

Asas ametoa ahadi
hiyo Leo wakati akifungua kikao cha baraza kuu la UWT Wilaya ya kilolo.

Alisema kuwa
lengo la kusaidia jumuiya hiyo ni kuitaka ijitegemee pia kuwa na miradi yake.


Kwani alisema
ameona ni vema kuiwezesha jumuiya hiyo kupata ndoano kuliko kuipa samaki na kwa kipindi chake chote cha miaka mitano atakayokuwepo madarakani ataichangia
jumuiya hiyo kiasi cha shilingi milioni 5 kwa ajili ya ujenzi huo

"Ahadi yangu
nitapaswa kuiweka katika maandishi ili familia yangu ijue pale nitakapo
tangulia mbele za Haki ahadi hii iweze kutekelezwa na familia maana hatujui la
kesho"

Hata hivyo
alipongeza jitihada za UWT wilaya ya Kilolo kwa kuwa na mipango ya kimaendeleo
kwa jamii tofauti na vyama vya upinzani.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages