Balozi
wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem azindua kisima cha maji cha 61
Wilayani Kigamboni, Dar es salaam kwa ajili ya Shule ya Msingi ya
GEZAULOLE yenye wanafunzi 868 na Shule ya Sekondari ya Ibnu Rushdy yenye
wanafunzi 250 ikiwa ni mwendelezo wa utekelezezaji wa mradi wa ''
KISIMA CHA MAJI KATIKA KILA SHULE'' ulioanzishwa na Ubalozi wa Kuwait
mwanzoni mwa mwaka 2017. Hafla ya uzinduzi wa kisima hicho ilihudhuriwa
pia na Diwani wa Sumangila Francis M. Chichi, Mwenyekiti wa Serikali ya
Mtaa Maziku Luhemega, Mwenyekiti wa CCM Gezaulole Masiku Lupa, Mwalimu
Mkuu Maryam Shaaban pamoja na wakaazi, walimu na wanafunzi wa Shule
hiyo. |
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269