Breaking News

Your Ad Spot

Mar 2, 2018

JUKWAA LA WANAWAKE SOMANGILA, KIGAMBONI, LAZINDULIWA LEO, ANGEL AKILIMALI AWATAKA WANAWAKE WAJASIRIAMALI KUZALISHA BIDHAA BORA KUKIDHI SOKO

Na Bashir Nkoromo, Kigamboni
Wanawake wajasiariliamali wametakiwa kutengeneza au kuuza bidhaa zenya ubora wa viwango vinavokubalika ili kuvutia wateja kununua bidhaa zao na kuongeza masoko ndani na nje ya Nchi.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Somangila, Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Katika uzinduzi huo uliofanyika Uwanja wa Dege katika Kata hiyo  Angela alisema mbali na na bidhaa bora kuhamasisha wanunuzi na kuongeza masoko ndani na nje ya Nchi boa bidhaa hizo zinaweza kumudu ushindani katika soko.

Alivishauri vikundi vya Wanawake wajasiriamali kwenda kuomba mikopo kwenye Benki ya Wanawake Tanzania ambayo alisema ni benki yenye mikopo ya riba nafuu.

Uzinduzi wa Jukwaa hilo ni sehemu ya shamrashamra za Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo yatafanyika mapema mwezi huu.
 Wanawake wa vikundi vya Wajasiriamali wakiandamana kutoka kwenye Ofisi yao kwenda kwenye uwanja wa Dege, kwenye Uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata ya Somangila Wilayani Kigamboni, Dar es Salaam, leo
 Mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Somangila, Kigamboni Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali (kulia) akiwa na baadhi ya Viongozi wa Jukwaa hilo wakati wakipokea maandamano ya Wanawake Wajasiriliamali kwenye uzinduzi wa Jukwaa hilo, leo
 Viongozi wa Vikundi mbalimbali vya Wanawake Wajasiriamali na Jukwaa la Wanawake wakiwa tayari kupokea maandamano ya wanawake Wajasiriamali. Kushoto ni Mgeni Rasmi Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM angel Akilimali akipunga mikono
 Viongozi wakimwayamwaya kupokea maandamano hayo 
 Mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali akisoma moja ya mabango waliyokuwa nayo Wanawake Wajasiliamali walipowasili Uwanjani kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Somangila.
 Diwani wa Kata ya Somangila Wilayani Kigamboni, Francis Chichi (kulia) akionyesha umahiri wa kusakata muziki pamoja na Kinamama wakati wa Uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata hiyo, leo
 Mwanamke Mjasiriamali wa kutengeneza vifaa vya ujenzi Amina Zakumera (kushoto) akimpatia maelezo ya utaalam wake Mgeni Rasmi Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali (Wapili kulia) alipokuwa akikagua bidhaa za Wanawake wajasiriamali wakati wa uzinduzi wa jukwaa la Wanawake wa Kata ya somangila, Kigamboni, leo 
 Angel Akilimali akipata maelezo kuhusu bidhaa za mwanamke Mjarismali  Winifrida Jafari (kushoto) wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata ya Somanga, Kigamboni leo. Wapili kushoto ni Mjasiriamali Joha Amour wa Joha Fashion.

 Angel Akilimali akitazama mkeka uliotengenezwa na Mwanamke Mjasiriamali Jawa Maulidi (kushoto)
 Angel Akilimali (kushoto) akimuuliza Mwanamke Mjasiriamali jinsi anavyotengeneza bidhaa zake.
 Angel Akilimali na Diwani Chichi wakinywa togwa kwenye banda la maonyesho la Mwanamke Mjasiriamali, wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata ya Somangila, Kigamboni. 
 Wanawake wajasriamali wa Kata ya Somangila wakijimwayamwaya kucheza muziki kufurahia uzinduzi wa Jukwaa lao, leo
 Mtendaji wa Kata ya Somangila Munna Msafiri akitambulisha viongozi wa vikundi mbalimbali na Jukwaa la wanawake kutoka maeneo mbalimbali
 Viongozi wa Majukwaa ya Wanawake kutoka kata mbalimbali za Halmashauri ya Kigamboni wakitambulishwa
 Diwani wa Kata ya Somangila Ndugu Chichi akifanya harambee ya uchangiaji wa fedha kutunisha mfuko wa Jukwaa la wanawake katika kata yake.
 Mkuu wa Polisi Kata ya Somangila Mwakila Chile akizungumza baada ya kutambulishwa na Diwani Chichi
 Mwekezaji wa Mbutu Beach Resort katika Kata ya Somangila Prakash Naran akiungana na Wanawake wajasiriamali kusakata muziki wakati wa sherehe za uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Somangila
 Mwekezaji wa Mbutu Beach Resort katika Kata ya Somangila Prakash Naran akicheza ngoma na msanii wa kikundi cha Vijana wa Somangila wakati wa Sherehe hizo za uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Somangila 
 Mgeni rasmi katika Sherehe za uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake Kata ya somangila Kigamboni Angel Akilimali akifurahia vijana walivyokuwa wakionyesha uhodari wa kucheza sarakasi wakati wa sherehe hizo
 Kijana akiwa kihwa chini miguu juu, tena hewani wakati akicheza sarakasi wakati wa sherehe hizo
 Wasani wa kikundi cha sanaa cha Vijana wa Smangila wakionyesha uhodari wa kucheza sarakasi wakati wa sherehe hizo
 Mgeni rasmi katika sherehe za Uzinduzi wa Jukwaa la wanawake wa Kata ya Somangila, Kigamboni, Angel Akilimali akinadi kiatu alipoendesha mnada wa vitu mbalimbali vya wanawake wajasriamali wakati wa sherehe hizo
 Mwekezaji wa Mbutu Beach Resort katika Kata ya Somangila Prakash Naran akikitazama kwa makini kiatu hicho baada ya kukubali kukinunua kwa sh 50,000
 Angel Akilimali akihutubia Wakati wa Sherehe za uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata ya Somangila, Kigamboni, leo
  Angel Akilimali akihutubia Wakati wa Sherehe za uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake wa Kata ya Somangila, Kigamboni, leo
 Angel Akilimali akipongezwa na MC katika sherehe hizo
 Angel Akilimali akiwa na mtunza Fedha wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Kigamboni Pili Doto mwishoni wa uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake kata ya Somangila
 Angel Akilimali (kulia) akizungumza jambo na Mkurugenzi wa New Life Queen Bahati mwishoni mwa sherehe hizo
 Angel Akilimali akiwa na baadhi ya Wanawake wajasiriamali
Mgeni Rasmi katika sherehe za uzinduzi wa Jukwaa la wanawake Kata ya Somangila, Kigamboni Dar es Salaam, Angel Akilimali akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Jukwaa hilo katika kata mbalimbali za Kigamboni na Viongozi wa vikundi vya Wanawake wajasiriamali wa kata hiyo baada ya uzinduz leo. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages