Breaking News

Your Ad Spot

Mar 5, 2018

MAKATIBU WAKUU 15 KUTAFUTA SULUHU ZA CHANGAMOTO ZINAZOKABILI ZIWA MANYARA NA TISHIO LA KUKAUKA KWAKE

Lango Kuu la Kuingilia Hifadhi ya Taifa ya Lake Manyara ambapo Makatibu Wakuu zaidi ya 10 kutoka Wizara mbalimbali wametembelea kujionea hali ya tishio lililopo la Ziwa Manyara na Maeneo ya Shoroba .
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akitoa neno la ukaribisho kwa Makatibu Wakuu  kutoka Wizara mbalimbali katika kikao cha Mawasilisho ya Taarifa ya Tishio la kutoweka kwa Ziwa Manyara na Maeneo ya Shoroba .
Mwenyeji wa Ziara ya Makatibu Wakuu,Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali ,Gaudence Milanzi akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho.
Kaimu Meneja wa Ikolojia katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara ,Yustina Kiwango akifanya Wasilisho la Taarifa kuhusu tishio la kutoweka kwa Ziwa Manyara,Maeneo ya Shoroba na Mitawanyiko ya Wanyama Tarangire -Manyara kwa Makatibu Wakuu hao.
Kaimu Meneja wa Ikolojia katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara ,Yustina Kiwango akitoa maelezo kwa Makatibu Wakuu hao .
Miongoni mwa Majengo yaliyokuwa yakitumika kama Vyoo katika Hifadhi ya Taifa ya Lake Manyara likionekana kuharibika baada ya maji ya Mvua yaliyoambatana na Mawe zilizonyesha miaka michache iliyopita. 
Muonekana wa majengo mengine yaliyokuwa yakitumika kama vyo kwa wageni waliotembelea Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara baada ya kuharibika kutokana na Maji hayo ya Mvua.
Sehemu ya Ndege ambao ni kivutio kimojawapo kikubwa katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara ambao hutegemea pia uwepo wa Maji katika maeneo hayo ambayo kwa sasa yameanza kukauka kutokana na Uharibifu wa Mazingira unaofanywa na Binadamu .
Mkuruenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi (Mwenye kofia) akiwaonesha Makatibu Wakuu waliotembelea Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara maeneo ya Ziwa Manyara ambayo yameanza kukauka.
Eneo moja wapo la Vivutio vya Utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara likionekana kuanza kukauka kutokana na Athari za kimazingira zinazosababishwa na shughuli mbalimbali za kibinadamu zikiwemo ,Kilimo Uchimbaji wa Madini katika maene ya jirani na Ziwa hilo. 
Viabda vinavyotumiwa na Wachimbaji wa Madini katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara .
Moja ya Mtambo unaotumika katika shughuli za Uchimbaji wa madini katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara ukiwa umehifadhiwa katika eneo mojawapo la Uchimbaji.
Maeneo ambayo shughuli za Uchimbaji wa Madini umekuwa ukifanyika katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara .
Kijana akifanya shughuli ya uchekechaji wa Mchanga katika moja ya mito inayo peleka maji Ziwa Manyara ,shughuli hi imekuwa ikifanyika kwa lengo la kujipatia Madini ana ya Dhahabu ,Hata hivyo zoezi hili linatajwa kuwa moja ya Uharibifu wa Mazingira unaochangia kukauka kwa Ziwa Manyara.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali ,Gaudence Milanzi akiwanesha baadhi ya Makatibu Wakuu namna ambavyo athari za kimazingira zimeanza kuonekana katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara .
Baadhi ya Makatibu Wakuu wakitizama kwa mbali Ziwa Manyara.
Makatibu Wakuu wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Hifadhi za Taifa (TANAPA) na wa serikali katika mikoa ya Arusha na Manyara mara baada ya kihitimisha ziara hiyo.
Na Dixo Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini .

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages