Breaking News

Your Ad Spot

Sep 9, 2018

ZOEZI LA KUSAJILI WAKAAZI WA ZANZIBAR KATIKA MFUMO WA KIELEKTRONI (E-ID CARD) LAANZA

 Zoezi la uandikishaji wananchi wa Zanzibari katika mfumo wa kidigitali limeanza rasmi  Sept 8, 2018 katika Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati Unguja. Ambapo idadi kubwa ya wananchi imejitokeza kujiandikisha ili waweze kupata kitambulisho ya kielektroniki (E-ID CARD). 

Mapema wiki hii rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein alizindua Vituo vya Usajili wa Vitambulisho vya Mzanzibar na Uzinduzi wa Uimarishaji Mfumo wa Usajili kielektroniki hafla iliofanyika katika viwanja vya Ofisi hiyo Dunga Wilaya ya Kati Unguja.

Ambapo lengo la mfumo huo ni kuifadhi taarifa katika mfumo wa kisasa ili kurahisisha hupatikanaji huduma na taarifa pindi zinapohitajika. Zoezi hilo limeanza katika vituo tofauti vya Skuli ya Dunga Kiembeni,kituo cha Dunga Bweni katika skuli ya Maandalizi na kituo cha Skuli ya Mpapa vyote katika Mkoa wa Kusini.
Wananchi wakiendelea kuandikishwa.
Mwitikio wa wananchi ulikuwa ni mkubwa sana.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages